Writen by
sadataley
10:42 AM
-
0
Comments
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe ameachiwa saa saba na robo usiku wa kuamkia leo baada ya kuhojiwa na Jeshi la Polisi.
Mbowe alikamatwa jana Jumatatu jioni wakati akienda kujisalimisha polisi
na kupekuliwa nyumbani kwake kabla ya kuhojiwa hadi alipoachiwa usiku.
Ofisa habari wa chama hicho, Tumaini Makene amethibitisha taarifa za kuachiwa mwanasiasa huyo kuwa ni za kweli.
Hata hivyo, taarifa iliyosambazwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum
Mwalimu kupitia mitandao ya kijamii imesema kuwa chama hicho kitatoa
taarifa zaidi juu ya tukio hilo leo.
“Tunawashukuru wote kwa sala, maombi na subira na hivyo kuhitimisha
salama saa kumi za mwenyekiti wetu kuwa chini ya Jeshi la Polisi katika
Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam,” Mwalimu amesema.
Chanzo: Muungwanablog
No comments
Post a Comment