Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, June 17, 2017

Fanya hivi pale mtoto mchanga anapopatwa na kwikwi.

Kwikwi ni kitu cha kawaida kutokea hasa umri unavyozidi kwenda. Na mtoto mchanga yupo kwenye hatari zaidi ya kupata kwikwi, pia hata ndani ya mfuko wa kizazi kuanzia wiki ya sita mtoto huweza kupata kwikwi. Kwikwi hizi huweza kuwepo kati ya dakika moja hadi saa bila kuleta madhara yoyote kwa mtoto.

Chanzo cha kutokea kwa kwikwi kwa mtoto.
Kwikwi husababishwa na kusinyaa kwa misuli kitaalamu diaphragm(contraction or irritation of diaphragm) ambayo hutenganisha kifua na tumbo, na kwa madaktari bingwa wa watoto wanasema pia kwikwi huweza kusababishwa na aina ya vyakula, vyakula hivyo ni kama (maziwa anayonyonya kutoka kwa mama, au maziwa ya kopo) mara nyingine inaelezwa ya kwamba kutokea kwa kwikwi kwa mtoto husababishwa na na joto la mtoto linaposhuka sana.

Kwikwi huwa hatari sana pale inapotekea mara kwa mara na kutopata nafuu, na kusababisha mtoto kushindwa kunyonya, kula na kulala. Hivyo inapotekea hali hii mpe mtoto maji kidogo, huku ukimsugua mgongo. Unaweza kutumia Grip water. Mpe mtoto chakula akiwa ametulia, na jaribu kubadilisha mkao wa mtoto, na kumtuliza mtoto na hali hii inaweza kuisha.
 mpe mtoto Grip water kwa kipimimo cha 0.5mm

Ukiona hali hii haiiishi ni vyema kwenda kwa daktari bingwa wa watoto mapema iwezekanavyo, ili uweze kupata msaada wa kitaalamu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment