Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, February 8, 2017

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma afananishwa na Trump.

media
Gazeti la Mail and Guardian lamfananisha rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma na Trump
Ofisi ya Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, imejibu kwa hasira baada ya gazeti la The mail and Guardian kuchapisha makala inayomfananisha na rais wa Marekani Donald Trump.
Gazeti la Mail na Guardian limechapisha makala yenye kichwa cha habari "Trump na Zuma wabaya zaidi kuliko waongo."
Ofisi ya Rais inaona kuwa makala hiyo imechapishwa kinyume na "mikataba ya uandishi wa habari na uhuru wa kujieleza."
Bunge la Afrika Kusini linafikiria kupendekeza sheria inayoadhibu lugha ya chuki kwa viongozi wa nchi. Matusi kwa rais bila shaka itakua ni uhalifu.
Ikumbukwe kwamba Rais Jacob Zuma anakabiliwa na kampeni kadhaa za kumchafua tangu kashfa iliyoitwa "Nkandla" iibuke.
Rais Zuma anashtumiwa hasaa katika chama chake cha ANC, chama tawala nchini Afrika Kusini.
Rais wa Afrika Kusini alipatikana na hatia ya kuwa alitumia Euro milioni 20 ya hazina ya Afrika Kusinikwa kujenga makazi yake binafsi katika eneo la Nkandla.
Alitakiwa kulipa sehemu ya fedha ya fedha hizo.RFI
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment