Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, April 15, 2017

NINI MAANA YA PASAKA KATIKA MAISHA YA WAKRISTO NA JAMII NA JINSI YA KUITUNZA



Image result for askofu Mbedule 
Askofu Lucas Yudah Mbedule
Ufafanuzu wa Kibiblia kuhusu
1.        Siku ya Mitende  na Juma Takatifu
2.        Usiku wa Kuwekwa(Kuanzishwa) Chakula cha Bwana.
3.        Ijumaa Kuu( Mashtaka,Hukumu,Mateso na Kifo cha Yesu Kristo
4.        Jumapili ya Pasaka( Yesu Amefufuka)
5.        Jumatatu ya Pasaka( Yesu Mfufuka anajidhihirisha kwa watu wote)
Neno Pasaka linaanza tangu Agano la Kale (Kutoka 12;18-20) Katika historia ya Ukombozi wa Wana wa Israel Misri. Huko walikotumikishwa na Farao na  Wa Misri. Neno Pascha ni neno la Ki ebrania lenye maana ya Kupita,kuvuka kuondoka na na neno ambalo kwa Kiingereza ni PASSOVER, Kwa maana ileile kupata,aukuvuka na neno hilo lilitohole wa moja kwa moja kwenda kwa lugha ya Kiswahili na kuitwa “Pasaka” toka Ki ebrania na Kiingereza na kulitumia kama neon la Kiswahili( Luka 22:1) hapa Pasaka inaakisi tukio la kukombolewa kutoka Misri.
Hivyo Wayahudi waliiadhimisha siku hii kila Mwaka wakati wa  Mwezi wa NISSAN ambao ni kati ya Mwezi Machi na Aprili( maana yake unaanzia (Tarehe 15 Machi hadi 15 April hivi kipindi hiki huitwa Nissan yaani kinagusa miezi miwili pamoja.
Mfano kalenda ya Kiyahudiinasomekahivi
1.        Nissan    ni   Mwezi wa Kwanza  (  Machi – April)
2.        Iyar     ni Mwezi wa Pili  (  April – Mei)
3.        Sivan  ni Mwzi wa Tatu ( Mei – Juni)
4.        Tammuz  ni Mwezi wa Nne ( Juni – julai)
5.        Av   ni MweziTano ( Julai – August)
6.        Elul  NI Mwezi wa Sita ( August – Septemba)
7.        Tishri  Mwzi wa Saba ( Septemba – Oktoba)
8.        Cheshvan Mwezi wa Nane ( Oktoba –Novemba)
9.        Kislev  ni Mwezi wa Tisa ( Novevemba – Desemba)
10.      Tevet  ni Mwezi wa Kumi ( Desemba – Januari)
11.      Adari(Leap years only) Mwezi wa  kumi na moja( Januari-Februari)
12.      Adari ( unaitwa adaribeit  in leap years)  Mwezi wa kumi na mbili( Februari – Machi)
Hivi ndivyo Wayahudiwa navyoisoma miezi yao( kwao miezi ni majira siyo siku. Kwa hiyo majira husika yakibadilika ndivyo hutaja Mwezi. Linganisha na sisi kipindi cha Mvua za vuli, hatuangalii Tarehe tunaangalia majira.
Na hivyo hata wakati wa Yesu amaeikuta ikiadhimishwa(Mathayo 26;1-5).
Waliiadhimisha kukumbuka Mateso yao kule Misri, na jinsi walivyokombolewa na Mungu kwa njia ya Mtumishi wake Musa( Kutoka 3:7ff)
Katika Kutimiza Mpango wa Wokovu Yesu anaingia Katika Historia ya Wokovu wa Wayahudi ili Wokovu wa watu wote.
Kwa hiyo tunapoangalia maana ya Maadhimisho haya, tunapaswa kuangalia kwanza Mwanzo wa Juma linalotangulia Pasaka, Tunaingizwa kuchunguza( habari hii inasimuliwa na Injili zote  Nne yaani Mathayo,Marko,Luka na Yohana) tofauti na habari ya kuzaliwa ambapo Marko hazungumzi kuzaliwa.
Yesu anavyoingia Yerusalemu Kama Mfalme, lakini kwa Jicho la Wayahudi wanamwona ni Mfalme wa Kidunia.
Siku ambayo huitwa siku ya Mitende au siku ya Matawi, aina hii ya majani ilitumiwa na Wayahudi kwa mapambo Katika sikukuu hasa wakiwapokea watawala wao  Zaidi kwa Kaisari pekee.

Pia mshtuko mwingine Katika hisia za viongozi wa serikali ya Kirumi ni Wimbo ambao Yesu anaimbiwa ..Hosia na Mbarikiwa ajaekwajina la Bwana….(……..)Inaonekana pia uliongeza hasira kwao kwa kuwa huyu anayeimbiwa na kupokelewa  kwa heshima kubwa hana cheo wala nafasi Katika utawala wa Kirumi.

Maadhimisho ya Siku ya Alhamisi ya Pasaka
Kama siku ya Kuwekwa au kuanzishwa Meza ya Bwana (Lord’s Supper) na Kukanwa kwa Yesu na kuachwaPekee yake.
Wakristo tunakutana kwa maana ya kujiimarisha Kiroho kwa kutafakari  upendo wa Mungu( Yohana 3:16) kumtoa Mwana wake, hapa siku tunaona na kujikumbusha hatua kwa hatua tena za awali za  Maandalio ya   Yesu kuagana na wanafunzi wake , Yesu kuwaombea, tena kuanzishwa kwa Chakula cha Bwana( Mathayo 26:26)
Ndiyo maana makanisa  yote( mainline Churches) huadhimisha tendo hilo kama Sakramenttakatifu (Eucarist).
Kwa Mkristo kuiheshimu kuitunza  siku hii ingepaswa kuwa tabia ya Muhimu kwa kuwa ndiyo kiini cha Historia ya Ukombozi ambao Mungu aliupanga kwa Mwanadamu.(Yn 3;16)

Maadhimisho ya Ijumaa Kuu (Good Friday)
Kama kukumbuka(Commemorate) Mashitaka,hukumu,Mateso na Kifo.Ni siku muhimu kwa kutafakari mashtaka, Hukumu,Mateso na kifo cha Yesu.
Kuiadhimisha siku hii ni kuingia kwa undani kuona uzito wa tendo la Yesu Kufa badala yetu sisi tulio stahili kufa. Watu wengi hawachukulii uzito unaostahili IBADA hizi labda kwa kukosa maelezo sahihi kwa kuwa kadiri siku zinavyokuja uzito wa Ibada hizi unapungua kabisa.
Pengine Nyimbo na Mahubiri hayaandaliwi kutuingiza kwa undani kutafakari maana ya Siku hii Katika maisha ya Kiroho.

Pia ni nafasi ya kutafakari ni jinsi gani vyombo vyetu vya kutunza sharia na haki za watu kama mahakama na vyombo vya ulinzi vinatoa haki kwa raia wake.( rejeahukumu ya Yesu kubambikiziwa mashitaka)
Vyombo vyetu vya Makanisa ni kwa jinsi  gani vin ajali na kutunza hali  Katika kuamua mashauri yao
Muhimu: Siku ya Alhamishi ni (Commemoration not Celebration) Kuadhimisha kwa Kukumbuka siyo Kusherehekea.) Ni tendo kubwa hapo la Kukumbuka. Maana yake tunaadhimisha kwa kukumbuka. Mfano tunaadhimisha kumbukumbu ya kifo cha ndugu tuliyempenda( to Commemorate) lakini katika Jambo la furaha , tunasherehekea( to  Celebrate). Ibada ya Kufufuka hiyo ina mambo yote mawili( Tunakumbuka na Kusherehekea Ushindi wa Yesu kutoka Mauti. Ikor 15:55-5.

Maadhimisho ya Pasaka yenyewe
Jumapili inayofuata Ijumaa
Kama siku  ya Wakristo kukumbuka kufufuka kwa Yesu Kristo kutokaMauti na Kaburi.Ushindi dhidi ya Kifo na dhambi,.
Siku hii muhimu wake Mkubwa ni Ushindi kwa kuwa Yesu kuwa amefufuka toka kaburi, Mungu amemfufua ni siku ya furaha kwa Wakristo na matumaini ya maisha ng’ambo ya kifo cha kimwili. Yesu anjidhihirisha kuwa ni mshindi wa Mauti (Ikorinth 15;55-56).
Kiini kikuu: Ni furaha, Haleluya Bwana Amefufuka Kwelikweli, Watu waondolewe hofu na mashaka yote dhidi ya Shetani dunia na Kifo. Katika Ibada hizo za furaha waoneshwe matumaini yaliyong’ambo ya maisha haya kuwa kuna Maisha mapya.
Watu waoneshwe jinsi Yesu alivyo na nguvu dhidi ya maumivu na Shida zetu. Lakini pia waonyeshwe kuwa Yesu anatenda mwenyewe lakini pia anatumia vyombo vya kidunia ili kuendelea maisha ya hapa Duniani pia( Yohana 9:7 Yesu anataka kuonyesha kuwa Hospitali zetu pia ni vyombo vya kutunza uhai na maisha yetu. Yesu anataka watu waishi duniani vizuri na kufurahia uumbaji kwa kuwafufua waendelee na maisha yao ya kila siku, lakini pia Yesu anaruhusu pia kifo ilitufike ng’ambo ya pili yaani uzima wa milele( Yohana 11;43)


Jumatatu ya Pasaka
Kama maadhimisho ya Kukumbuka Yesu Mfufuka anavyojitokea na kujidhihirisha kwa watu Katika maisha yao ya kawaida kama (a) kutembeanao Safarini (b) kuzungumza nao(c) kulanao(d) kubarikinyumba na maisha yao.Lk 24:13-35)
Kleopa na Mwenzake asiyejui kana jina walitembea na Yesu kitambokirefu, walizungumza naye kitambo kirefu hata pia walimdharau kwanini amechelewa kujua habari zilizo pomjini?  Luka 24:17-18, Wakasimama wakakunja nyuso zao; Wakamwuliza  Yesu;……. Je wewe pekee yako u Mgeni Katika Yerusalem, hata huya juiyaliyotukia?
Pia habari hii inaonyesha kuwa tunaposafiri inaonekana wako wanaojulikana kwa majina na Ukristo wao lakini wengine hawajulikani hata kama wapowapo(Kleopa anatajwa Katika kujadiliana na Yesu.
Wewe Jina lako linafahamika wapi Zaidi kwa Yesu au nje ya Yesu?
Siku hii ni ya muhimu pia ni maalumu kwa kutakari Jinsi Yesu Mfufuka ambavyo anajitokeza kwa mtu mmojammoja kama Mungu pamoja na watu wakeyaaniEmanuel ( Luka 1:23)
Ndiyo tunakutana na Yesu Katikati ya wasafiri,Yesukatikati ya mazungumzo ya kawaida na Yesu katikati ya familia na anashiriki chakula baada ya kukaribishwa.
Fundisho  la Ibada hii ya Jumatatu ni  kuwa  Bwana Yesu anavunja na kuvukamipaka na vikwazonakuingia Katika maisha ya mtu mmojammoja na vikundivya watu(Mfano wa jumuiandogondogo Katika maisha ya Kanisa).
Lakinitunajifunza kuwa;
1.        Watu wanawezakujisahau na kwendamwendamrefu wa maisha bila kumsikiliza na kumwelewa Yesu wa kumpanafasi.
2.        Familia inaweza kwenda mwendo mrefu wa maisha bila kumkaribisha Yesu na kumpa nafasi Yesu ili awe Baraka kwa familia.
3.        Kanisa pia linaweza kwenda mwendo mrefu bila kumkaribisha Yesu wa kumshirikisha Yesu.
Tunaweza kumhubiri,kumwimba na kumtaja Yesu lakinitusimfahamu wala kumsikiliza.
Msingi mkubwa wa Sikukuu hizi Katika Kanisa  na Jamii unapaswa kuwa ni kama KIOO cha kujiangalia na kujitathimini hali yetu ya wakati husika kufuata mazingira husika kifamilia,kijamini,kisiasa na kiutamaduni.Ujumbe mkuu wa  majira ya Pasakani AMANI. Mungu awabariki wote ilitukafanyike viwanda vya kuzalisha amani. Naawape Mwanga wa kufahamu mambo hayo kwa ajili ya kukua ki roho.
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu Amen.
Imeeandaliwa na Askofu Lucas Mbedule Judah (KKKT DAYOSISI YA KUSINI MASHARIKI MTWARA)


« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment