Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, February 8, 2017

WAFANYABIASHARA WA DAWA ZA KULEVYA WAKAMATWA IRINGA ...

mkuu wa  mkoa wa Iringa Amina Masenza 
Dawa  za kulevya 
                                 Kamanda  wa polisi mkoa  wa  Iringa (RPC) Julius Mjengi
..............................................................................................................
Na MatukiodaimaBlog 
BAADA  ya mapambano  ya  vita  dhidi ya  madawa ya  kulevya  kuendelea  kuchukua  kasi katika  mkoa  wa Dar es Salaam kwa  watuhumiwa  mbali mbali  kukamatwa , mkuu wa  mkoa  wa Iringa Amina Masenza ametangaza  mapambano  dhidi ya  dawa  za  kulevya  mkoani hapa  na kuwa  tayari mapambano yameanza  kuzaa matunda  baada ya  watuhumiwa 19  kukamatwa wakiwemo wafanyabiashara wa  dawa  za kulevya  
Akizungumza na mwandishi  maalum wa mtandao  wa matukiodaimaBlog   mkuu  huyo  wa mkoa  alisema  kuwa  hata kabla ya agizo la Rais Dkt  John Magufuli juzi mkoa  ulianza kupambana na madawa ya  kulevya  pamoja na matukio mbali mbali yanayohusiana na matumizi ya  dawa  za  kulevya kama  unywaji  pombe muda wa kazi oparesheni  ambayo  imefanywa kwa nguvu  kubwa  na jeshi la  polisi .

“ Pamoja na  kuwakamata  watuhumiwa mbali mbali ila  mkoa  umeendelea  kuandaa utaratibu  wa  kuwasaidia  waathirika  wa dawa  za  kulevya kwa kuwatafutia nafasi  ya matibabu  na kupitia hao  wataweza  kupata mtandao mzima  wa wauzaji  na  waingizaji wa dawa za  kulevya  mkoani Iringa …..tunaendelea kutekeleza agizo la  Rais kwa  vitendo  zaidi hatutalala  wala kukubali vijana  wetu  kuendelea  kuharibiwa akili kwa matumizi ya dawa  za  kulevya “

Kamanda  wa  polisi  wa  mkoa  wa Iringa Julius Mjengi akizungumza na  waandishi wa habari jana  juu ya utekelezaji wa agizo hilo la mapambano  dhidi ya  dawa  za  kulevya  alisema kuwa  jeshi la  polisi  limeendelea na msako mkali  wa  dawa za  kulevya kwa kuwakamata watuhumiwa 19 wa  dawa za kulevya .

Kamanda Mjengi  alisema kuwa kati ya  watuhumiwa hao   watuhumiwa  14  ni mateja  ambao wameathirika kwa utumiaji wa dawa  za  kulevya na watuhumiwa  5  ni wafanyabiashara  wa  dawa  za  kulevya .

“ Tulianza  kuwakamata  watumiaji wa dawa  za  kulevya ambao baadhi yao ni mateja (waathirika)  na baada ya  hapo mateja  hao  waliweza  kuwataja  wauzaji  hao watano ambao  tumewakamata na tunaendelea  kuwahoji mtandao  mzima  wa uingizaji wa dawa  za  kulevya mkoani Iringa “

Hata  hivyo  alisema kwa  sasa ni mapema  kutaja majina  ya  watuhumiwa hao wa dawa  za kulevya kwani bado  wanaendelea  na zoezi la kuwahoji ili kupata mtandao  mzima wa wauzaji wa dawa za kulevya na  kabla ya  kuwafikisha mahakamani wote kwa pamoja .

Alisema  kuwa  watuhumiwa hao  wamekamatwa katika maeneo mbali mbali ya Manispaa ya  Iringa likiwemo eneo la Miyomboni , Mwembetogwa , Mlandege , Mshindo , Ipogolo ,kitanzini na Kihesa  na  kuwa  zoezi  la kuwakamata  wote  waliotajwa  kwa kujihusisha na matumizi ya dawa  za  kulevya ama uuzaji  linaendelea .
Kuhusu  aina ya dawa  ambazo  walikuwa  wakiuza alisema watuhumiwa hao wote hakuna  aliyekamatwa na  dawa  za  kulevya na katika mahojiano wote  wanadai kuwa walikuwa  wakijihusisha  na biashara   hiyo zamani  ila kwa  sasa  wameiacha  kabisa .
Kamanda huyo  alisema mbali ya  kutokutwa na  ushahidi bado hawataachiwa  huru watafikishwa mahakamani  kujibu tuhuma  zao .
Aliwataka  wananchi wa mkoa  wa Iringa  kutoa ushirikiano kwa  jeshi la  polisi kwa kuwafichua  wale  wote wanaojihusisha na biashara ama matumizi ya  dawa za kulevya kwani  alisema oparesheni  hiyo inayoendelea  ni mkoa  mzima wa Iringa 
Chanzo Matukio Blog
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment