Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, April 5, 2016

Magufuli kuzuru Rwanda ziara ya kwanza nje

Hiyo itakuwa ziara ya kwanza ya Magufuli nje ya Tanzania tangu Oktoba Rais wa Tanzania John Magufuli amepangiwa kufanya ziara yake ya kwanza nje ya nchi hiyo tangu kuingia madarakani mwaka jana. Dkt Magufuli anatarajiwa kuzuru nchi jirani ya Rwanda Jumatano na Alhamisi, kufuatia mwaliko kutoka kwa Rais Paul Kagame. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wizara ya mambo ya nje ya Tanzania, Dkt Magufuli na Bw Kagame watafungua daraja la kimataifa la Rusumo na kituo cha huduma za pamoja mpakani katika mpaka wa Tanzania na Rwanda. Kagame kuiga Magufuli katika matumizi Baadaye, wataelekea Kigali ambapo watafanya mazungumzo ya pamoja. Dkt Magufuli pia ataweka shada la maua katika makumbusho ya mauaji ya kimbari ya Rwanda 1994 mjini humo. “Ikizingatiwa kwamba hii ndiyo ziara yake ya kwanza nje ya nchi tangu achukue madaraka Oktoba 2015, ziara hii inaashiria umuhimu ambao Tanzania inaweka katika kuimarisha uhusiano wake na majirani zake.” Rais Magufuli amekuwa mapumzikoni nyumbani kwake eneo la Chato, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment