Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, April 5, 2016

Uwanja wa ndege wa Brussels wafunguliwa tena

Ndege ya shirika la ndege la Ubelgiji kuelekea katika mji wa Ureno wa Faro imeondoka katika uwanja wa ndege wa Brussels Jumapili ikiwa ni ndege ya kwanza ya abiria kuruka tokea miripuko ya kigaidfi Machi 22. Ndege ya shirika la ndege la Ubelgiji kuelekea katika mji wa Ureno wa Faro imeondoka katika uwanja wa ndege wa Brussels Jumapili ikiwa ni ndege ya kwanza ya abiria kuruka kutoka uwanja huo tokea miripuko ya mabomu ya kujitowa muhanga katika ukumbi wa kuondokea hapo Machi 22. Usalama katika uwanja huo umeimarishwa kwa taratibu mpya za ukaguzi wa abiria. Ndege nyengine mbili zimepangwa kuondoka baadae katika kitovu hicho cha usafiri wa anga barani Ulaya ambapo kilikuwa kikishughulikia safari 600 kwa siku.Baadae ndege ya shirika la ndege la Ubelgiji moja itaelekea Athens Ugiriki na nyengine itakwenda mjini Turin,Italia. Arnaud Feist Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uwanja wa Ndege wa Brussels ameziita safari hizo za Jumapili kuwa "ishara ya matumaini " kufuatia "siku za kiza kabisa katika historia ya usafiri wa anga nchini Ubelgiji." Pia amewashukuru wafanyakazi wote kwa ushujaa wao. Akizungumza katika hafla iliofanyika katika uwanja huo amesema "ziada ya kuwa ni uwanja wa ndege wamezidi kuwa familia iliyoungana." Uharibifu katika uwanja huo ulikuwa mkubwa sana kutokana na miripuko miwili ya kujitowa muhanga karibu na eneo la ukaguzi wa abiria lililokuwa limejaa watu siku kumi na mbili zilizopita na kuuwa watu 16 na kujeruhi wengine wengi kutoka sehemu mbali mbali duniani. Mripuko mwengine siku hiyo hiyo umetokea katika kituo cha reli ya chini ya ardhi mjini Brussels na kuuwa watu wengine 16. Kundi la Dola la Kiislamu limedai kuhusika na miripuko yote hiyo. Feist amesema uwanja huo mkubwa kabisa nchini Ubelgiji utakuwa umerudi katika uwezo wa kufanya kazi kwa asilimia ishirini ifikapo Jumatatu na kuweza kuwahudumia abiria 800 kwa saa. Hapo Jumamosi alisema anataraji huduma kamili katika uwanja huo zinaweza kurudishwa kufikia mwanzoni mwa mwezi wa Julai wakati wa msimu wa mapumziko wa majira ya kiangazi. Hatua mpya za usalama katika uwanja huo zinakusudia kupunguza nafasi za kurudiwa kwa mashambulizi hayo. Polisi Jumapili walikuwa wakikaguwa magari kabla ya kuwasili.Hema kubwa limewekwa nje ya ukumbi wa uwanja wa ndege huo kukaguwa vitambulisho vya wasafiri, hati za kusafiria na mikoba yao kabla ya kuruhusiwa kuingia ndani ya jengo la uwamnja huo. Eneo la kuegesha magari nje ya ukumbi wa uwanja wa ndege limefungwa na maafisa wamesema kutakuwa hakuna usafiri wa reli na ule wa umma kuelekea katika uwanja huo katika kipindi cha hivi karibuni. Washambuliaji wa kujitowa muhanga waliingia katika eneo la ukaguzi uwanjani hapo wakiwa na mikoba iliosheni mabomu na misumari na miripuko hiyo imesababisha kuanguka kwa dari la uwanja huo na kuvunja madirisha. Mashambulizi hayo yamezusha mjadala mkubwa miongoni mwa maafisa wa usafiri wa anga katika nchi nyingi juu ya iwapo kufanya ukaguzi wa kawaida katika sehemu za kuingilia kwenye kumbi za uwanja wa ndege.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment