Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, January 25, 2015




SIKU YA CCT (JUMUIYA YA KIKRISTO TANZANIA

CHUO KIKUU DAR ES SALAAM
MAHUBIRI YA 25.01.2015

ZABURI 133

Leo ni siku ya CCT Jumuia ya Makanisa Tanzania leo imetimiza miaka 81, lilianzishwa 25/01/1934 likiwa na lengo la kuboreshwa kuanzisha shughuli nyingine zinazojibu mahitaji ya watu. Hivyo tupo kusherehekea kazi na utume ambao wenzetu walikaa na kuona kuna haja ya kukaa na kushirikiana pamoja kwa sisi tulio katika mwamvuli mmoja.(Waprotestant). 

Kwa sasa mwenyekiti wake ni Askofu Dr. Alex Gehaz  Malasusa na Katibu Mkuu ni Mchungaji  Dr. Leonard Mtaita. Jumuiya hii ina tunu zake (core value za  CCT) –Love (upendo), Compassion (matendo ya huruma), Unity(Umoja) and Ecumenism, Professionalism (Utaalam), Faithfulness (Ukweli), Transparency (Uwazi), Accountability (Uwajibikaji), Stewardship (Utoaji), Trustworthy(Uaminifu) ,Integrity(Uwezo)  na Honesty

Wanachama wake ni (CCTchurch members)Evangelical Lutheran Church in Tanzania(ELCT),Anglican Church Tanzania(ACT),Moravian Church of Tanzania(MCT),Africa Inland Church Tanzania (AICT),Mennonite Church in Tanzania (MCT),Baptist Church in Tanzania (BCT),Salvation Army,Presbyterian of East Africa (PEA),Bible Church Tanzania, African Brotherhood Church,Church of God in Tanzania na Evangelistic Church of Mbalizi.

Vyama vilivyopo chini ya CCT ni Bible Society of Tanzania, Tanganyika Refugees Service, Youth Men’s Christian Association ,Young Women’s Christian Association, Africa Enterprise Evangelistic ,Life Ministry, Mission Aviation Fellowship, Emmanuel International, Summer Institute of Linguistic, Dodoma Christian Medical Center, Mennonite Central Committee na Compassion International Tanzania

Makanisa yaliyo chini ya CCT (Chaplaincy)umoja huo ni Chuo Kikuu Dar es Salaam (UD), Mzumbe, Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) na Chuo Cha Kilimo Morogoro(SUA).

Wayahudi  waliamini kuwa Yerusalem ilikuwa ni kila kitu, huu ni mji wenye milima mingi sana na ndipo  palipojengwa hekalu.  Palikuwa ni mlimani hivyo ilikuwa ni sehemu ya juu kabisa. Na katika Hekalu kazi yao kubwa  ilikuwa ni kwenda kuabudu tu.

Mlima Herimoni upo Kaskazini ya Yerusalemu, inayoonekana juu ya Yordani, kulikuwana mvua kubwa sana na barafu.Maji yake hutiririka hadi Yeriko. Wayahudi leo hii wanaimba wimbo huu ili kuonyesha furaha kubwa kwani  walikuwa na uhakika wa kukutana na Mungu wao.

Zaburi hii inawapa Tumaini na Baraka kwa wote waliomtegemea na inafungua mlango wa Imani na Baraka hasa ikizingatiwa kuwa hekalu lilikuwa juu kabisa na kupelekea wao kuamini ndiyo Injili ilipoanza kutawanyika.  Bwana anaandaa familia ya waaminio. Umoja huleta vionjo na unyevu uliopo katika mlima huu ni kama Roho Mtakatifu amebeba utakaso wa Wana wa Mungu. Na hii inatokana na ukweli uliopo kuwa hakuna anayeweza kupima upendo wa kimahusiano  uliopo kati ya  Mungu na watoto wake.

Ili maisha yawe bora na yenye furaha ni lazima upendo uwepo.  Imani si lazima uone kwa macho moja kwa moja  kilichopo ni kukubali tu; Heri wale ambao wanamuamini lakini hawajauona. Ni kama vile Yesu anavyomwaambia Tomaso katika Yohana 20:29.

Ni ndipo tunachokiona kuwa Injili inatawanyika na kutengeneza familia ya Kikristo. Na leo tuna mamilioni ya Wakristo na kumwamini Yesu Kristo katika Umoja, Tumaini, na Upendo. Upendo ni mbegu na zaburi hii imejikita sana katika kuyaweka pamoja makabila ya Israel. Na haiishii hapo inafika na katika familia zetu, jamii zetu na Kanisa. (2 Korintho 13:11, Waefeso 4:1-6, Wafilipi 2:2-8 na wakolosai 3:14-15).

Jambo kubwa tunaloliona katika Zaburi hii ni umoja katika Baba [Mungu] anayejidhihirisha kwetu kwa njia ya Yesu Kristo. Ndugu [kaka-kindred] “Brother” si kwa ajili ya ndugu wa damu lakini ni kwa ajili ya wale wanaounganishwa na Neema ya Mungu. Na jambo kubwa hapa ni sisi ni kumwabudu Mungu na kuwaleta wengine kwa Yesu kwa njia ya Uinjilishaji.

Hivyo na sisi leo tuone kama tupo kwa ajili ya imani hiyo na kuwafanya wengine wamwanini Mungu  na kuuona umoja ambao ulianzishwa na Yesu. Hasa wale waliopo katika mabonde[dhambi, wahitaji walioonewa,wasiopata haki za msingi].

Tunaona mafuta yakitumika kama kimiminika kinachoweza kutelemka. Na kuona ubarikio[ ordination] wa Aaron Walawi 8:12.  Hivyo wale wote waliobarikiwa wamewekewa mafuta ya Aaron juu yao. Kwetu sisi mafuta ni ishara ya kuabudu[worship],kufunga[feast],sherehe ndani ya Ushirika na Mungu.

Ujio wa Yesu kwetu sisi ni kuja kutupa maji sisi tulio na kiu ,Yesu amekuja kwa ajili ya wale wasio na chakula, malezi, haki na upendo wapate yote hayo Yesu anatupenda sote. Yesu asingalikuja tungekuwaje.

Yesu amekuja kutupa Tumaini yeye amekuja kwa ajili yetu. Sisi ni wanae tu, familia moja ya Kikristo ya waaminio. Umoja wa hapa duniani ndiyo utakao tupeleka Mbinguni.

Tunapoelekea katika uchaguzi  Mkuu

Nchi yetu iko katika njia panda inaweza kupiga hatua kubwa ya maendeleo na hali ya maisha ya wananchi wote kuboreka kutokana na ugunduzi wa gesi asilia, kuendelea kupanuka na kuboreka kwa huduma za  kijamii, kupanuka kwa sekta binafsi na fursa nyingi za biashara, jitihada kubwa za ujenzi wa miundombinu na mambo mengine mazuri yaliyofanywa na serikali za awamu zote.

Ipo hatari ya taifa letu kupasuka kutokana na dalili za mpasuko wa kidini, mmomonyoko wa maadili kwenye jamii, kuporomoka kwa imani ya wananchi kwa dola ufa katika muungano na umaskini na tofauti kubwa ya kipato baina ya watu na hali ya kukata tama miongoni mwa wananchi. Uongozi madhubuti, uongozi wa zama za sasa  unahitajika.

Rais ajaye ana kazi kubwa zaidi ya kusimamia umoja wanchi yetu na usalama, amani na utulivu kuliko viongozi waliopita. Lazima kiongozi ajae ayajue kwa kina mazingira ya sasa, awe ameyaishi, na kutambua mahitaji yake.

Nchi yetu ni kubwa sana na ina takribani makabila 120 makubwa na madogo ina ukubwa wa ardhi wa kilomita za mraba laki tisa na nusu, ni muungano wan chi mbili; nusu ya wananchi wake wakiwa wamezaliwa ndani ya uongozi wa Rais Mkapa na Kikwete na vijana chini ya miaka 35 ni asilimia karibu 80, na wengi wao wakiwa hawana ajira.

Kuna viashiria vya nyufa kati ya wakulima na wafugaji,wachimba madini wadogo na wawekezaji wakubwa, Wakristo na waislamu, wabara na wazanzibari, matajiri na maskini wa kutupwa.Rais wa Awamu ya Tano awe ni mtu mwenye kuzitambua changamoto hizo na kuwa na mkakati wa kuzitatua.

Inategemea  wajihi yaani character, wa kiongozi mwenyewe. Hivyo, wajihi wa mgombea unapaswa kujibu maswali yanayoletwa na changamoto hizi.Tumeshuhudia miji ikikua kwa kasi kubwa na umaskini ukiongezeka mijini hali iliyozaa uhalifu na uvunjifu wa amani.

Tunae soma tusome kwa bidii na tusitegemee sana kuajiliwa tuanze kutafuta na kuziona fursa. Tupo hapa chuo Kikuu kwa sababu ya Baraka na upendo wa Mungu. Tupo hapa kwa kusudi la Mungu tu. Yesu awe rafiki yetu siku zote.

Ni dhahiri kwamba tofauti ya kipato baina ya walionacho na wasionacho imeongezeka. Hivyo tunaposherehekea na kuadhimisha sikuu hii tuombe roho ya umoja iwe kwetu ili amani, upendo na uvumilivu tuliokuwa nao tuendelee kuwa nao daima. Siku ile ya mwisho tutakuwa kundi moja na mchunga mmoja. (Mahali ni Pazuri 244 na TMB324),hivyo tuishi kwa kupendana na kusaidiana.

Ameni

Imeandaliwa na

MCHUNGAJI KURWA SADATALEY

VITABU REJEA

MacDonald William Believers Bible Commentary

Adeyemo Tokunboh The African Bible Commentary: A one Volume Commentary written by 70 Africa Scholars

New Interpreters Bible vol. VI (Nashvile Abingdom, 1996)

James Limburg, Psalms (Louisville, KY: Westmister John Knox, 2000)

Richard Clifford, Psalms 1-72 (Nashivile: Abingdon, 2002).

Paul J. Achtemeier, ed. Harper Collins Bible Dictionary (HarperSanFrancisco, 1996), 41
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment