Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, April 5, 2016

Zuma aponyoka kura ya kutokuwa na imani naye

Zuma anusurika kura ya kutokuwa na imani naye Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amepenyoka kura ya kutokuwa na imani naye bungeni. Zuma alipata kura kutoka kwa wabunge 233 wanaomuunga mkono dhidi ya 143 za wabunge ambao hawakuwa na imani naye. Awali naibu spika alikuwa amewataka wabunge wapaze sauti hadharani kuhusu iwapo alikuwa anaunga mkono kura ya kutokuwa na imani au la. Hata hivyo upinzani ulishinikiza kura hiyo iendeshwe kwa njia halisi sawa na kura zingine. Wachanganuzi wa maswala ya kisiasa nchini Afrika kusini walikuwa wanatarajia matokeo hayo kutokana na idadi kubwa ya wabunge wa chama tawala cha ANC. Bunge la Afrika Kusini liliamua kusikiza na kujadili hoja ya kumng'oa rais Jacob Zuma kufuatia shinikizo kutoka kwa vyama vya upinzani. Spika wa bunge la Afrika Kusini bi Baleka Mbete, alikubali hoja hiyo ijadiliwe kufuatia mahakama ya juu ya Afrika Kusini kumpata rais Zuma na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka yake. Chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) kinachoongozwa na Julius Malema kilienda mahakamani kikitaka rais Zuma ashurutishwe kulipa fedha zilizotumika kinyume cha sheria kufanya ukarabati katika makazi yake ya Nkandla. Upinzani uliwasilisha kesi mahakamani baada ya bwana Zuma kupuuza uamuzi wa mwaka 2014 kuwa alinufaika kutokana na ukarabati wa nyumba yake na kwamba alistahili kulipa pesa zilizotumiwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment