Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, March 27, 2016

Wagombea warushiana matusi Marekani

Wagombea wa urais nchini Marekani kupitia tiketi ya chama cha Republican Ted Crus na Donald Trump walirushiana cheche za matusi katika mjadala Wagombeaji wawili wa Urais wa chama cha Republican nchini Marekani wamegombana vikali na kurushiana matusi juu ya wake zao. Seneta wa Texas, Ted Cruz, amemlaumu mpinzani wake, mfanyabiashara Donald Trump kwa kuzusha uvumi kuwa yeye alikuwa mzinifu na kumdanganya mkewe, Heidi. Bwana Cruz alisema uvumi huo ni takataka na akasema kuwa anaelewa kuwa uvumi ulianzishwa na Bwana Trump ambaye alisema hastahili kuwa Rais. Bwana Trump alisisitza kuwa hakuhusika vyo vyote na uvumi huo. Mjadala wa wagombea urais nchini Marekani Mapema juma hili, Bwana Trump alimlaumu Seneta Cruz kwa kuweka picha za mkewe, Melania, akiwa uchi kwenye mtandao ili kumharibia sifa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment