Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, March 27, 2016

Rais kuongoza kwa muhula mmoja Benin

Rais mpya aliyechaguliwa nchini Benin, Patrice Talon, anasema anataka kupunguza muda wa rais anaoweza kuongoza, kuwa muhula mmoja tu wa miaka mitano. Bwana Talon, ambaye alimshinda waziri mkuu katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais juma lilopita...amesema muda mfupi wa uongozi utasaidia kile alichoelezea kuwa rais kuridhika na kutokuwa na hima akiongoza muda mrefu. Alisema atakuwa na mawaziri 16, karibu nusu tu ya idadi ya zamani. Rais anayestaafu, Thomas Boni Yayi, ametumikia mihula miwili. Msimamo wa rais mpya wa Benin ni tofauti na viongozi wengine wa Afrika, ambao hivi karibuni wameongeza muda wao wa uongozi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment