Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, March 31, 2016

Wafadhili wasitisha ufadhili kwa bajeti ya Tanzania

Mataifa 10 ya Magharibi yamesema hayataendelea na ufadhili wao kwa bajeti ya serikali ya Tanzania. Baadhi ya nchi hizo ni Sweden na Ireland. Nchi hizo zinaendelea na msimamo huo ikiwa ni siku chache baada ya shirika la utoaji misaada la serikali ya marekani (MCC) kuondoa msaada wake wa dola 472 za ufadhili wa miradi ya maendeleo kwa Tanzania. Bodi ya MCC ilisema hatua yake ilitokana na mzozo kuhusu uchaguzi wa kisiwa cha Zanzibar na utekelezwaji wa Sheria ya Uhalifu wa Mtandao. Mataifa yaliyositisha ufadhili wao kwa bajeti ya Tanzania hata hivyo hayajaeleza sababu ya kufanya hivyo. Ubalozi wa Sweden umethibitisha kwamba taifa hilo limesitisha ufadhili wake kwa bajeti ya Tanzania, lakini ukasisitiza kwamba hatua hiyo haihusiani na yaliyojiri katika uchaguzi wa visiwa vya Zanzibar. Tanzania yasikitika kunyimwa pesa za MCC Uchaguzi wa Zanzibar waikosesha hela Tanzania "Mwaka uliopita, Sweden ilikuwa moja ya nchi zilizositisha ufadhili wake kwa bajeti ya Tanzania kutokana na tuhuma za ufisadi kuhusiana na sekta ya kawi [na mkataba wetu na serikali ulifika kikomo mwaka jana],” ubalozi huo umeambia BBC. “ Sweden inafurahishwa na juhudi za serikali kukabiliana na ufisadi na iko tayari kuanzisha majadiliano na serikali ya Tanzania na wafadhili wengine kuhusu mikakati ya kufadhili bajeti ya Tanzania siku zijazo.” Ubalozi wa Ireland pia umethibitisha kwamba ni kweli taifa hilo halifadhili tena bajeti ya Tanzania. Ufadhili wake wa mwisho ulitolewa mwaka wa kifedha wa 14/15, malipo ambayo yalifanyika Juni 2015 na kwa sasa hakuna malipo yaliyoratibiwa ya mwaka wa kifedha wa 15/16. "Mpango ulimalizika Juni 2015 na hakuna mipango mingine ya kutoa ufadhili kwa bajeti (ya Tanzania),” ubalozi wa nchi hiyo umesema. Karibu theluthi moja ya bajeti ya Tanzania ilitegemea msaada mwaka uliopita, kwa hivyo hatua ya nchi hizo ni pigo kwa mipango ya maendeleo ya serikali mpya.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment