Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, March 22, 2016

Obama na Castro wajibizana Cuba

Rais Obama na mwenyeji wake Raul Castrol Rais Barack Obama na mwenyeji wake Raul Castrol wamejibizana kuhusu suala la haki za binadamu na vikwazo vya kibiashara baina ya Marekani na Cuba. Hata hivyo Rais Obama amehimiza Cuba kuendelea na mageuzi ya kisiasa na haki za binadamu kama inataka kurejesha ambao kwa miaka mingi umedorola baina ya mataifa hayo mawili. Katika siku ya pili ya ziara yake ya Kihisitoria nchini Cuba, rais Obama amesema kuondolewa kwa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya taifa hilo la Kikomonisti kutategemeana na uharaka wa mataifa hayo mawili kuondoa tofauti zao hasa katika suala la haki za binadamu. Obama amesema kuwa Marekani haioni kama Cuba ni tishio kwa Marekani na kwamba ziara yake nchini humo ina lengo la kuweka misingi mipya kati ya mahusiano baina ya nchi hizo mbili. Rais Obama baada ya mazungumzo ya mjini Havana na mwenyeji wake Raul Castro, amesema kutokuwepo harakati za kupigania haki za binadamu nchini Cuba ni jambo litakalo mpatia ugumu kushawishi bunge la Congress kuondoa vikwazo vilivyopo dhidi ya Cuba.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment