Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 29, 2015

Kiongozi wa kundi la Taleban amefariki

Habari kutoka kwa serikali ya Afghanistan zimeiambia BBC kuwa kinara mkuu wa kundi la wapiganaji wa Taliban, Mullah Omar amefariki. Lakini habari hizo bado hazijathibitishwa rasmi na kundi hilo. Kwa miezi kadhaa kumekuwepo na tetesi kuhusiana na kifo cha Mullah Omar. Kifo hicho kimetokea wakati ambapo serikali ya Afghanistan ilikuwa inajiandaa kuanza mashauriano ya amani na kundi hilo la Taliban. Waandishi wa habari wameitwa na serikali ili kuhudhuria kikao cha wanahabari jijini Kabul, ambao unatazamiwa kufanyika muda mchache ujao. Taarifa nyingine zinasema kuwa huenda alifariki miaka kadhaa iliyopita. Chanzo:BBC Swahili
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment