Writen by
sadataley
10:04 AM
-
0
Comments
Waziri Mkuu mstaafu Mh Edward Lowassa leo amejiunga na UKAWA kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika hafla iliyohudhuriwa na waandishi wa Vyombo Mbalimbali vya habari. Hafla hiyo ambayo imehudhuriwa na Viongozi wote wanaunda umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA akiwemo mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahimu Lipumba, Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa NCCR Maeuzi Mh James Mbatia na Mwenyekiti wa NLD Mh Emmanuel Makaidi.
Lowassa ambaye aliambatana na mkewe Mama Regina Lowassa wote walikabidhiwa kadi ya kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema na Mh Freeman Mbowe.
Katika Hotuba yake mara baada ya kutangaza kujiunga na Chadema Mh Lowassa ameongelea mambo mengi yaliyomshawishi kujiondoa CCM na kujiunga na UKAWA kupitia CHADEMA hosusani suala la mchakato wa kupata Mgombea Urais kupitia CCM lilivyotawaliwa na zengwe. Katika Hotuba yake Mh Lowassa amewaomba Watanzania wote wenye kulitakia mema Taifa Kujiunga na UKAWA kwa ajili ya kutimiza Safari ya Matumaini.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments
Post a Comment