Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, October 31, 2013

Syria yateketeza vifaa vya kemikali

Shirika la kimataifa la kusimamia matumizi ya silaha za kemikali, limesema kuwa Syria imetangaza kwamba vifaa vya kuzalisha, kuchanganyia na kujazia silaha za kemikali vimeharibiwa.
Wakaguzi wa kimataifa wa silaha za kemikali
Tangazo hili limetolewa siku moja kabla ya kumalizika kwa tarehe ya mwisho iliyowekwa na Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali duniani, OPCW.
Msemaji wa OPCW amesema silaha hizo zimewekwa lakiri ili kudhibiti matumizi yake.
Wakaguzi wa silaha hizo walitumwa Syria kufuatia tuhuma dhidi ya serikali ya nchi hiyo inayoshutumiwa kutumia silaha za kemikali katika maeneo ya raia.
Kwa upande wake Syria inakanusha shutuma hizo na badala yake imewashutumu wapinzani kuhusika na matumizi ya silaha za kemikali katika vita vinavyoendelea nchini humo kati ya majeshi ya serikali na waasi.
Mashirika ya ujasusi ya nchi za Magharibi, yatakuwa yanafuatilia kwa karibu tangazo la Syria la kuteketeza silaha zake za kemikali.
Ukaguzi huu ni makubaliano yaliyofikiwa kati ya Urusi na Marekani, baada ya Marekani kutishia kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya serikali ya Syria, kufuatia tuhuma hizo.
Kwa sasa vifaa hivyo haviwezi kutumika.
Syria imetakiwa kuharibu yenyewe silaha zake za kemikali ifikapo katikati ya mwaka 2014.

ICC yaahirisha kesi dhidi ya Rais Kenyatta

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imeahirisha kesi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika mahakama hiyo hadi tarehe 5 mwezi Februari mwaka 2014.
Uamuzi huu umetolewa huku AU ikifanya juhudi za kidiplomasia kutaka kesi hiyo kuahirishwa kwa mwaka mmoja
Uamuzi huo umefikiwa hii leo ikiwa siku moja kabla ya upande wa mashitaka kuashiria kuwa hawatapinga ikiwa kesi hiyo kuahirishwa kwa mwaka mmoja hadi Novemba mwaka 2014
Pia unakuja huku juhudi za kidipmolasia za viongozi wa Afrika kushinikiza baraza la usalama la Umoja wa Mataifa zikishika kasi kulitaka baraza hilo kukubali kesi dhidi ya Rais Kenyatta na naibu wake William Ruto kuakhirishwa.
Rais Kenyatta alikuwa ameiomba mahakama hiyo kuakhirisha kesi dhidi yake hadi Februari mwaka ujao huku upande wa mashitaka ukitaka ukahirishaji kutozidi Februari tarehe tatu mwaka 2014.
“Majaji wamekubaliana na upande wa mashitaka kuahirisha kesi dhidi ya Rais Kenyatta hadi Februari mwaka 2014 ili kuupatia upande wa mashitaka muda wa kutosha kufanya uchunguzi zaidi kutokana na tuhuma dhidi ya upande wa mashitaka kutoa taarifa zisizo za kweli, '' majaji walisema katika uamuzi wao.
Upande wa utetezi nao ulitaka tarehe ya kesi hiyo kuahirishwa ili majaji waweze kushughulikia baadhi ya malalamiko yao, kuhusu Kiongozi wa mashitaka kuhujumu mfumo wa kesi dhidi ya Kenyatta. Malalamiko hayo waliyawasilisha Oktoba tarehe kumi na kuwasilisha ombi la kutaka kesi dhidi ya Rais Kenyatta kufutiliwa mbali.

Wakenya washinikiza wabakaji wakamatwe

Mamia ya waandamanaji nchini Kenya wamewasilisha kwa polisi hati ya kutaka kukamatwa kwa watuhumiwa waliombaka msichana huyo wa miaka 16.
Liz alibakwa na watu waliomtupa kwenye shimo la choo na kumvunja uti wa mgongo
Msichana huyo alibakwa na kundi la wanaume na kutupwa katika shimo la choo ambapo alivunjika uti wa mgongo wake.
Wanaume wanaotuhumiwa kumbaka msichana huyo waliamrishwa na polisi kukata nyasi kama adhabu ya kitendo hicho.
Hati hiyo ya kutaka kuwafungulia mashitaka watuhumiwa wa ubakaji imetiwa saini na watu milioni 1.2 wakitaka watuhumiwa kukamatwa haraka na kuwafikisha mahakamani.
Waandamanaji hao wameelezea kukasirishwa na adhabu hiyo na kuhoji kwa nini polisi hawakufanya uchunguzi ili kumtendea haki msichana huyo.
Pia wanataka polisi waliowaadhibu washukiwa na kisha kuwaachilia, wakamatwe na kufunguliwa mashitaka.
Tayari wanawake milioni 1.2 wameunga mkono kampeini hiyo iliyoanzishwa na mwanaharakati Nebila katika mtandao wa kijamii wa Avaaz ulio na wanachama milioni ishirini na saba kote duniani na inaarifiwa idadi ya wanawake wanaopinga kitendo cha wabakaji na kile cha polisi kuwaadhibu kwa kukata nyasi, inaendelea kuongezeka.
Kampeini hii imekuja baada ya msichana Liz kubakwa na genge la wanaume sita ambao baadaye walimtupa ndani ya shimo la choo.
Liz alipata majeraha mabaya sana na hata kuvunjika uti wa mongo na sasa amelazimika kutumia kiti cha magurudumu na hadi sasa amefanyiwa upasuaji katika sehemu zake za siri.
Polisi waliwakamata watuhumiwa watatu kati ya sita waliodaiwa kumbaka msichana huyo, lakini baadaye wakawaachilia baada ya kuwaadhibu kwa kukata nyasi nje ya kituo cha polisi.

Wednesday, October 30, 2013

K.K.K.T DAYOSISI YAFANYA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA DAYOSISI; YAFANA HUKU WAJUMBE WAKIFURAHIA NAMNA NA JINSI DAYOSISI INAVYOKWENDA KASI KATIKA KUJILETEA MAENDELEO

























SHULE YA SEKONDARI YA KILUTHERI BOMALANG'OMBE INAYOMILIKIWA NA KKKT DAYOSISI YA IRINGA YAPATA MSAADA WA VITANDA TOKA MAREKANI
















K.K.K.T DAYOSISI YAFANYA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA DAYOSISI; YAFANA HUKU WAJUMBE WAKIFURAHIA NAMNA NA JINSI DAYOSISI INAVYOKWENDA KASI KATIKA KUJILETEA MAENDELEO