Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, April 27, 2017

Padri afunga ndoa

Miaka tisa baada ya kuvuliwa daraja la upadri wa Kanisa Katoliki, mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii, Privatus Karugendo amefunga ndoa na Rose Birusya.

Ndoa hiyo ilifungwa jana katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini hapa katika misa iliyoongozwa na Padri Stefano Kaombe.

Mapadri wa Kanisa Katoliki hawaruhusiwi kuoa na wanapoachishwa husubiri kibali maalumu kutoka kwa kiongozi wa kanisa hilo duniani.

Akiwa mwenye furaha, Karugendo alizungumza kwa simu na mwandishi wetu kwa dakika chache baada ya kufunga ndoa hiyo.

“Umepata wapi taarifa? Kumbe wamesharusha! Ndiyo tumetoka kanisani tunajiandaa kwenda ukumbini,” alisema Padri Karugendo ambaye pia huchangia makala katika gazeti hili.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment