Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, April 27, 2017

Hiki ndicho Kisiwa chenye upungufu wa wanawake

Kuna upungufu wa wanawake katika kisiwa cha Faroe.

Hivyobasi wanaume katika kisiwa hicho wanatafuta wanawake kutoka maeneo mengine kama vile mataifa ya Thailand na Ufilipino.

Lakini je ni changamoto gani zinazowakumba wanawake wanaoelekea katika kisiwa hicho.

Wakati Athaya Slaetalid alipoelekea katika kisiwa hicho ambapo kipindi cha majira ya baradi huchukua muda wa miezi sita alikuwa akikaa karibu na kikanza ama heater kwa jina la Kiingereza kwa siku nzima.

''Watu walikuwa wakiniambie niende nje kwa sababu kuna jua lakini nilisema'': ''Hapana niwacheni, nahisi baridi sana''.

Kuhamia katika kisiwa hicho miezi sita iliopita ilikuwa vigumu kwa Bi Athaya aliyekiri.

Alikutana na mumewe Jan alipokuwa akifanya kazi na rafikiye mmoja wa kisiwa hicho ambaye alikuwa ameanza biashara nchini Thailand.

Jan alijua mapema kwamba kumpeleka mkewe katika utamaduni huo, hali ya hewa itakuwa changamoto kubwa.

"Nilikuwa na wasiwasi kwa sababu kila kitu alichokiwacha nchini Thailand kilikuwa tofauti na kile alichokuja kuona katika kisiwa cha Faroe'', alisema.

''Lakini kwa sababu namjua Athaya nilijua ataingiliana na hali ya hewa''.

Kufikia sasa kuna takriban wanawake 300 kutoka Thailand na Ufilipino wanaoishi katika kisiwa cha Faroe.

Haionekani kuwa idadi kubwa lakini kisiwa hicho chenye idadi ya watu 50,000 sasa wanawakilisha watu walio wachache katika visiwa hivyo 18 kati ya Norway na Iceland.

Katika miaka ya hivi karibuni visiwa vya Faroe vimepata upungugufu wa wa idadi ya watu huku vijana wakiondoka ili kutafuta elimu na huwa hawarudi.

Wanawake wameamua kuishi ughaibuni.

Kulingana na waziri mkuu Axel Johannese, kisiwa hicho kina upungufu wa jinsia huku kukiwa na uchache wa takriban wanawake 2000 ikilinganishwa na wanaume.

Hatua hiyo imewafanya wanaume katika kisiwa hicho kutafuta wanawake katika maeneo mengine kwa mapenzi.

Wengi ijapokuwa sio wote wa wanawake hao wa bara Asia, walikutana na wanaume zao kupitia mtandaoni wengine kupitia mitandao ya kukutanisha wapendanao.

Wengine wamepatana kupitia mitandao ya wanandoa wa Asia na visiwa vya Faroe.

Kwa wale wanaowasili, utamaduni wa eneo hilo unaweza kuwaathiri.

Vikiwa ni miliki za Denmark, visiwa vya Faroe vina lugha yao na utamaduni wa kipekee hususan katika maswala ya chakula.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment