Na MatukiodaimaBlog
MVUA
kubwa zinazoendelea kunyesha wilayani Kilolo mkoani Iringa
zimeendelea kusababisha kero kubwa kwa watumiaji wa barabara za
wilaya hiyo kwa malori linayofika kubeba mazao kukwama huku mtu mmoja
akipoteza maaisha kufuatia basi la kampuni ya upendo kutumbukia mtoni
baada ya kushindwa kupanda mlima.
Wakitoa
kero zao kwa mbunge wa jimbo la Kilolo Venance Mwamoto aliyefanya
ziara ya ukaguzi wa miundo mbinu katika kata ya Kidabaga na Ng'uruwe
jana wananchi hao wakiwemo madereva waliokwama kwa zaidi ya siku
mbili katika eneo la Kidabaga walisema kuwa hali ya mvua
inayoendelea kunyesha imeendelea kuwatesa na hivi sasa wanalazimika
kulala njiani hasa mvua zinaponyesha wakiwa njiani .
Yohana
Sanga ni mmoja kati ya wasafirishaji wa mazao ya misitu katika
wilaya ya Kilolo alisema kuwa kutokana na mvua hizo hivi sasa
sehemu kubwa ya barabara za wilaya ya Kilolo zimekuwa hazipitiki
kirahisi hivyo kuiomba serikali ya wilaya ya Kilolo kuangalia
uwezekano wa kuboresha maeneo korofi ambayo yamekuwa hayapitiki hasa
kipindi cha mvua .
Alisema
kutokana na hali hiyo hasa sasa tayari mwanamke mmoja amepoteza
maisha na wengine zaidi ya watano ni majeruhi baada ya basi
walilokuwa wakisafiriki kuelekea mjini Iringa kushindwa kupanda
mlima wa Kidabaga na kuporomoka mtoni .
Diwani
wa kata ya Ng'uruwe Pancras Kihaga ambaye aliongozana na mbunge
huyo kukagua maeneo korofi ya barabara za Kilolo alisema kuwa maeneo
ambayo yanawatesa wasafiri na wasafirishaji ni pamoja na Kidabaga
na baadhi ya maeneo ya kata ya Ng'uruwe na hivyo kumuomba mbunge
huyo kusaidia kufikisha kilio hicho kwa Halmashauri ya Kilolo .
Mbunge
Mwamoto mbali ya kuwapa pole wahanga wa tukio la ajali ya basi
na ndugu wa mkazi wa jimbo hilo aliyepoteza maisha kwa ajali ya basi
bado alimtaka mhandisi wa ujenzi katika Halmashauri ya Kilolo kutoka
ofisini na kutembelea barabara hizo ili maeneo korofi kuyafanyia
kazi haraka badala ya kusubiri maafa .
Alisema
shida iliyopo ni uwajibikaji mbovu wa mhandisi wa ujenzi kila
wakati amekuwa akingoja kusukumwa ndipo atoke ofisini jambo ambalo
linapelekea wananchi kuendelea kuilalamikia serikali kwa kila
changamoto inapojitokeza .
Mbunge
huyo alisema kwa sasa ukarabati wa eneo hilo korofi la Kidabaga na
Ng'uruwe unaanza mara moja leo ili kuwezesha wananchi kupata
mawasiliano ya barabara ya uhakika .
|
No comments
Post a Comment