Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, November 30, 2016

Bashir: Ni rahisi kufanya kazi na Donald Trump

Rais Omar el Bashir wa Sudan

Image copyrightREUTERS
Image captionRais Omar el Bashir wa Sudan
Kiongozi wa Sudan Omar el Bashir amempongeza rais mteule wa Marekani Donald Trump akisema kuwa itakuwa rahisi kushirikiana naye, kulingana na gazeti la Emirati al Khaljee.
''Bw Trump anaangazia maslahi ya raia wa Marekani, ikilinganishwa na wale wanaozungumzia kuhusu demokrasia ,haki za kibinaadamu na uwazi'',alisema rais Bashir katika mahojiano na gazeti hilo.
Aliongezea kwamba: Tunaweza kushirikina na watu wenye sura mbili lakini huyu hapa mtu mwenye uwazi wa anajua anacholenga.
''Nina hakika itakuwa rais kushirikiana na Trump ikilinganishwa na wengine kwa sababu ni mtu anayeangazia maswala moja kwa moja na mfanyibiashara ambaye anaangazia maslahi ya anaoshirikiana nao'',alisema Bashir. 
Bashir ambaye anasakwa na mahakama ya ICC kutokana na mashtaka ya mauaji ya kimbari katika eneo la Drafur amekana mashtaka hayo.
Alichukua mamlaka mwaka 1989 kupitia mapinduzi na ameshutumiwa kwa kuwa na uongozi wa kiimla tangu wakati huo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment