Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, April 6, 2016

MUNGAI ACHARUKA AMFIKISHA ASKOFU MENGELE KWA MKUU WA KKKT

KUHANI MKUU WA KKKT Salaam KATIKA Jina la Bwana wetu Yesu Kristo BAADA ya kushindwa kukupata kwa SIMU; NAJITAMBULISHA kwako KUWA mimi ni Joseph James Mungai MKRISTO wa KKKT Jimbo la Mufindi. Tumewahi kukutana. Nilipokuwa Waziri wa Elimu nilimuwakilisha Rais Mkapa kwenye Sherehe YENU ya KUMUAGA Baba Askofu Kweka. Nimewahi kuwa Mbunge wa Wilaya ya Mufindi miaka 35. Nimewahi pia kwa nyakati tofauti kuwa Waziri wa Kilimo; Waziri wa Elimu; & Waziri wa Mambo ya Ndani ya NCHI. Aidha nimewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Ndani ya Kanisa nimewahi kuwa Mjumbe wa Halmashsuri Kuu ya Dayosisi ya Kusini. Kama MKRISTO wa kawaida niliyewahi, kwa Rehema ya Mungu, kuwa katika uongozi wa Nchi na wa Kanisa; na aidha kama Mzee wa Miaka 72; NAKUSHAURI UCHUKUE HATUA BILA KUCHELEWA YA kufanya mambo matano (5) yafuatayo: (1) Uzingatie Hoja za WAKRISTO wanaoteseka wa Jimbo la Mufindi tunaotengwa na kunyanyaswa na Askofu Mengele wa Dayosisi ya Kusini: (2) Uunde bila kuchelewa zaidi Tume ya Kanisa kwenda kusikiliza Hoja za kila upande (3) Utambue kuwa kwa wakati huu wa mpito Jimbo la Mufindi baada ya kunyanyaswa na kutengwa na Askofu Mengele limejihifadhi chini ya ulezi wa Dayosisi ya Iringa; (4) Kwa hiyo basi UAGIZE kuwa Dayosisi ya Kusini kutokana na yenyewe kulitenga Jimbo la Mufindi katika VIKAO VYA UAMUZI imepoteza uhalali wa kuamua jambo lolote kuhusu Jimbo la Mufindi mpaka mgogolo uliopo uishe chini ya UONGOZI WA KANISA. Kwa hiyo uamuzi wa jana wa kumuvua Uchungaji & Ukuu wa Jimbo Mchungaji Kipangula ni batili hata kwa Akili ya KAWAIDA. (5) Kwa NIABA y a KKKT uelekeze RASMI kuwa kwa sasa kondoo wa Jimbo la Mufindi tulionyanyaswa na kutelekezwa na Askofu Mengele wa Dayosisi ya Kusini TUKO chini ya ulezi wa Baba Askofu MDEGELA wa Dayosisi ya Iringa (DIRA) na HALMASHAURI KUU ya Dayosisi hiyo. Kwa SHALOM na kwa Heshima Kuu Nawasilisha. Aidha nawakumbusha Maaskofu wangu miliongoze Kanisa kwa nguvu ya Biblia na SIYO kwa nguvu ya Polisi kama Dola. Wa Salaam katika Jina Kuu la Yesu Kristo Joseph J Mungai M K R I S T O WA KKKT JIMBO LA MUFINDI MKOA WA IRINGA Cc: Baba Askofu MDEGELA Dayosisi ya Iringa Cc: Baba Askofu Mengele Dayosisi ya Kusini Chanzo:www.matukiodaima.co.tz
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment