Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, October 31, 2014

Askofu Angowi ahimiza amani, ataka kura maoni


Askofu mkuu wa Kanisa la Kilutheri Afrika Mashariki (KKAM), Jesse Angowi akihubiri katika uzinduzi wa Halmashauri Kuu ya Jimbo la Moshi mkoani Kilimanjaro jana. Picha na Daniel Mjema. 
Na Daniel Mjema, Mwananchi
Moshi. Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheri Afrika Mashariki (KKAM), Jesse Angowi amesema kutounga mkono kufanyika kwa kura ya maoni Aprili, 2015 ni kukaribisha machafuko nchini.

Hayo aliyasema wilayani hapa jana katika uzinduzi wa Halmashauri Kuu ya Jimbo la Moshi.

Aliwashauri viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuridhia kufanyika kwa kura hiyo na kuwaacha wananchi waamue kupigia kura kile wanachokitaka na siyo kuwalazimisha.

“Amani ikikosekana hata makanisa hayawezi kuhubiri injili. Hivi sasa kuna viashiria vya kutoweka kwa amani kabla hata ya mchakato wa kupigia kura Katiba Inayopendekezwa haujaanza.

“Ni lazima tutii kauli ya Rais Kikwete kwamba kura ya maoni itafanyika Aprili mwakani, vinginevyo ni kukaribisha machafuko. Hakuna Mtanzania ambaye yupo tayari kwa hilo,” alisema Askofu Angowi na kuongoza kuwa kanisa hilo linamuunga mkono Rais ili kura hiyo ifanyike.
Alisema ni vyema viongozi wa dini wakabeba jukumu lao la kutoa elimu kwa waumini kuhusu kuheshimu maagizo ya viongozi wao.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment