Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, October 30, 2014

DRC: Beni yagubikwa na mikasa ya vita  

Wanajeshi wa jeshi la Congo walikiwa msituni.
Wanajeshi wa jeshi la Congo walikiwa msituni.
               
Vita na mizozo vimezuka tena kuanzia katika mwa mwezi kwa kumi katika mji wa Beni nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya congo huku mamia ya watu wakipoteza maisha na maelfu kukoseshwa makazi yao.
Kwa mujibu wa mtetezi wa haki za binadamu Paluku Ngahangombi aliyoko katika mji huo na kushuhudia visa mbalimbali vinavyofanywa na wanaosadikiwa kuwa ni waasi wa ADF – NALU kutoka Uganda, anasema hali ya usalama inazidi kuwa mbaya.
Licha ya wananchi kuchukua sheria mkononi na kuanza kulala nje usiku wakiwasha moto, wakiwa na silaha kama vile mapanga na visu kujilinda na uvamizi wa waasi lakini bado ghasia zimeshamiri.
Usiku wa kuamkia  Jumatano waasi walivamia kambi ya jeshi katika mji wa Beni kwenye mtaa mkubwa wa Owicha na kufyatuliana risasi na wanajeshi wa serikali hali iliyopelekea askari mmoja  kupoteza maisha, na waasi wengi kujeruhiwa lakini  waliweza kutoroka.
Wakazi wa mji huo wameilaumu serikali na Jeshi la umoja wa mataifa MONUSCO kushindwa kushirikiana vyema kurejesha hali ya utulivu .
Paluku Ngahangombi anasema kina mama na watoto ndio wahanga wakubwa katika mapigano na visa vinavyofanywa na waasi kwa sababu hawawezi kujikinga kwa haraka.  Drc imegubikwa na vita, mizozo na mivutano ya aina mbalimbali kwa miongo kadhaa sasa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment