Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, September 30, 2014

Watu 270 walazwa kwa kunywa togwa

Na Joyce Joliga, Mwananchi
Songea. Watu zaidi ya 270 wa Kijiji cha Litapwasi, Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma wamelazwa wengi wao wakiwa na hali mbaya katika Zahanati ya Lyangweni na Hospitali ya Misheni ya St Joseph, Peramiho baada ya kunywa togwa inayosadikiwa kuwa na sumu.

Tukio hilo lilitokea juzi mchana kwenye sherehe ya Kipaimara kwa mtoto Dickson Nungu (14) na kuzua hofu kubwa kwa wakazi wa kijiji hicho ambao wanaonekana kutoamini kilichotokea.

Wingi wa wagonjwa hao umesababisha zahanati hiyo kuelemewa na kiasi cha wengine kulazwa chini kwenye udongo, barazani na kwenye miembe wakisubiri kupatiwa huduma ya kwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Mskhiela alisema polisi inawashikilia watu watatu kuhusiana na tukio hilo na vinywaji na mabaki ya chakula kilicholiwa vimezuiliwa huku sehemu ikichukuliwa sampuli ili kupelekwa kwa Mkemia Mkuu kwa uchunguzi zaidi.

Alisema waliopatiwa matibabu na kuruhusiwa ni watu 50 huku 190 wakiwa bado wanatibiwa Lyangweni na wengine 30 wakilazwa PeramihoHata hivyo, Kamanda Mshkhiela alisema walioathirika wanaendelea kuongezeka.
Mtoto Nungu, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Litapwasi, alipata Kipaimara hicho na mara baada ya chakula cha mchana, waalikwa walipewa pombe za kienyeji na wengine togwa. Baada ya muda mfupi, waliokunywa togwa na chakula, kila mmoja kwa wakati wake alianza kujisikia maumivu ya tumbo na kuharisha mfululizo huku wengine wakitapika damu.

Mama mzazi wa kijana huyo, Philbeta Ngonyani (36), ambaye pia amelazwa katika Hospitali ya Misheni Peramiho alisema: “Nimefikishwa hospitalini jana (juzi) saa nane usiku nikiwa sijitambui kutokana na maumivu makali kwa kuharisha mfululizo baada ya kunywa togwa.”

Akielezea tukio hilo alisema, anakumbuka siku moja kabla ya tukio, (Jumamosi iliyopita) yeye na wenzake (majirani) walishirikiana kupika togwa na walianza kazi hiyo saa sita adhuhuri na kumaliza saa 10 jioni na kisha kuiweka katika chumba kimoja ili ipoe kisha walimkabidhi ufunguo wa chumba hicho mtu aliyemtaja kuwa ni jirani yao, Ridhiwan Shawa ili siku ya sherehe mtu atakayehitaji kinywaji ampatie.
Alisema, juzi mchana mara baada ya mwanaye kutoka kanisani, waalikwa walifika nyumbani kwake wakiwa na watoto wao na baadhi ya ndugu na jamaa zao kwa ajili ya kujumuika kumpongeza kijana huyo na vyakula mbalimbali vilipikwa kama wali, pilau na ugali.

Alisema mara baada ya kula, vinywaji vilitolewa na kijana wake na baadhi ya watu walipatiwa soda na wengine waliomba pombe za kienyeji na togwa. “Waliokunywa pombe na soda hawakudhurika lakini waliokunywa togwa wengi walianza kusikia maumivu ya tumbo na kuanza kuharisha na kutapika mfululizo na wengine kuharisha damu, baadhi walirudi nyumbani na wengine walikimbilia zahanati.”

Alisema yeye, mumewe Ines Nungu pamoja na kijana wao mwingine, Matson wanaumwa tumbo, kuharisha na kutapika.

Jirani ambaye pia amelazwa, Aloysia Ngonyani alisema alifikishwa hospitalini hapo juzi usiku wa saa saba akiwa na maumivu makali ya tumbo huku akihara na kutapika baada ya kunywa togwa.
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Watu-270-walazwa-kwa-kunywa-togwa/-/1597296/2469654/-/129rcy5/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment