Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, September 29, 2014

Tibaigana: Wapinzani wana haki kuandamana


Alfred Tibaigana alipokuwa kazini siku chache kabla ya kustaafu. 
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake Buganguzi wilayani Muleba, Kamishna Tibaigana alisema suala la maandamano halikumsumbua kwa kuwa alielewa kuwa sheria inayaruhusu, hivyo alichokuwa akifanya ni kuwaita viongozi wa vyama vinavyotaka kuandamana na kufanya nao makubaliano ya namna maandamano hayo yanavyopaswa yafanywe kabla ya kuyaruhusu.

“Pengine hiyo ndiyo sababu sikuwahi kushambuliwa kwa maneno ya kejeli au matusi na wanasiasa kwa kuwa sikuwahi kuzuia maandamano yao bila sababu na hata kama kulikuwa na sababu niliwaita na kuwaeleza na tulikubaliana.

“Kikubwa ni kujenga tabia ya kuwaita viongozi wa waandamanaji na kujadiliana nao, vinginevyo wanaweza pia hata kukufikisha mahakamani wakipinga kuzuiwa maandamano yao,” alisema Tibaigana ambaye alikumbana na sakata la kudai maandamano wakati akiwa Kamanda kwenye mikoa ya Tanga, Arusha na Dar es Salaam.
“Nilikuwa nawaita viongozi nakaa nao tunakubaliana. Hata kama ningeambiwa na kiongozi gani nisitoe kibali, kama hakuna sababu za kweli, nilikataa kwa kuwa kisheria mimi ndiye nawajibika kama vyama vikishtaki. Ili uzuie maandamano unapaswa kuwa na sababu za msingi ambazo ukiwaeleza waandamanaji wanakuelewa.”

Tibaigana anakumbuka jinsi CUF kilivyoandaa maandamano makubwa kushinikiza kuundwa kwa serikali ya mseto visiwani Zanzibar baada ya kutoridhishwa na matokeo ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005, lakini anasema kutokana na msimamo wake, haikuwa vigumu kwake kuruhusu jambo hilo.

 “Wakati wa uongozi wangu CUF ilikuwa na nguvu sana, lakini mimi sikuwa na tatizo nao. Walipotaka kibali cha kuandamana niliwapa bila woga na tuliishi vizuri,” anaeleza Tibaigana.

Vuguvugu la maandamano pia lilitanda wakati wa maandalizi ya ziara ya Rais wa zamani wa Marekani, George Bush nchini kutokana na wasomi na baadhi ya wanaharakati kutaka kufanya maandamano kupinga vitendo vya taifa hilo kubwa dhidi ya raia wa Palestina na sehemu nyingine ambako wananchi wasio na hatia walikuwa wakiuawa.

“Nilichofanya ni kukutana nao na kuwaeleza njia ambazo wangeweza kutumia katika maandamano hayo na hali ilikuwa shwari,” alisema Kamanda Tibaigana.

Katika kipindi chake cha uongozi wa Polisi Dar es Salaam, Kamanda Tibaigana pia alikumbana na vurugu za kidini ambazo zilisababisha askari mmoja kupoteza maisha, lakini anasema kwa kushirikiana na wadau wengine, walijipanga na hali ikawa shwari.
Alivyomng’ang’ania Ditopile

Moja ya matukio makubwa wakati akiwa Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam ni tukio la mkuu wa zamani wa Mkoa wa Tabora, Ditopile kumuua dereva wa daladala baada ya kutokea kutoelewana barabarani, hali iliyolazimu sheria kufuata mkondo wake. Jeshi la Polisi lilitakiwa limkamate mkuu huyo na kumfikisha mahakamani.

Ditopile alituhumiwa kufanya mauaji hayo Novemba 5, 2006. Akidaiwa kumuua kwa kumpiga risasi dereva wa daladala, Hassan Mbonde. Alikamatwa na kufikishwa mahakamani, lakini alifariki dunia Aprili 20, 2008 wakati kesi yake ikiendelea.
Kwa habari zaidi ingia Tibaigana: Wapinzani wana haki kuandamana
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment