Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, September 28, 2014

Jeshi la Marekani: Tunadhoofisha Islamic State nchini Syria

    
Ndege za kivita zikishambulia ngome za Islamic State
Ndege za kivita zikishambulia ngome za Islamic State  

Na Victor Melkizedeck Abuso
Jeshi la Marekani linasema mashambulizi ya angaa dhidi ya wapiganaji wa Kiislamu wa Islamic State nchini Syria yanadhoofisha wapiganaji hao baada ya vituo vya mafuta walivyokuwa wanadhibiti kuteketezwa.

Hata hivyo, Mkuu wa Majeshi Jenerali Martin Dempsey amesema mashambulizi ya angaa pekee hayawezi kutegemewa kuwamaliza kabisa wapiganaji hao nchini Syria na Iraq.
Aidha, Jenerali Dempsey amesema suluhu la kisiasa linahitajika nchini Iraq na Syria ili kupata amani ya muda mrefu katika nchi hizo mbili.
Siku ya Ijumaa, wabunge nchini Uingereza nao walikubali jeshi lao kujiunga na Marekani, Ufaransa na mataifa mengine ya Ulaya na kutoka Umoja wa Kiarabu kuwashambulia wapiganaji hao.
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Chuck Hagel (Kushoto) akiwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Martin Dempsey (Kulia)

Katika hatua nyingine, Marekani inasema wapiganaji wa jeshi huru la Syria linahitajika kupambana na wapiganaji hao wa Islamic State ardhini ili kudhibiti kabisa ngome za wapiganaji hao.
Zaidi ya Mataifa 40 yamejiunga na Marekani kuongoza mashambulizi dhidi ya wapiganaji hao ambao wanaedelea kusababisha mauaji ya raia na kuchukua maeneo zaidi.
Mwanajeshi wa Iraq

Siku ya Ijumaa, Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov alishtumu mashamabulizi ya angaa nchini Syria bila ya kuishirikisha Moscow.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment