Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, August 31, 2014

Hali hairuhusu kupata Katiba


Mchungaji Antony Lusekelo akisisitiza jambo alipokuwa akiongea na waandishi wa Mwananchi, kanisani kwake Ubungo Kibangu jana. Picha na Kelvin Matandiko. 
Na Goodluck Eliona na Fidelis Butahe, MwananchiWakati Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakitarajiwa kuendelea na vikao mjini Dodoma kesho, Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Antony Lusekelo, amesema kuwa hali ya kisiasa hairuhusu nchi kupata Katiba Mpya kwa sasa, akishauri Bunge hilo kusitishwa hadi baada ya uchaguzi mkuu mwakani.
Lusekelo pia ameonya wajumbe wa Bunge hilo akisema iwapo wataendelea na mchakato huo, Katiba itakayoandikwa itakataliwa na wananchi baadaye hivyo kuwa wamepoteza muda na fedha za walipakodi bure.
Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu ofisini kwake jijini hapa juzi, Mchungaji Lusekelo alisema kuwa Mchakato wa Katiba Mpya, umevurugika kutokana na wanasiasa kujiona miungu watu na kukataa kusikiliza ushauri wanaopewa.
“Kwa upande wangu, kama viongozi wangekuwa wanatusikiliza, mchakato huu usingefika ulipofika leo. Hii misukosuko isingetokea, wanasiasa wetu wana tatizo hilo. Ni miungu watu, wana shingo ngumu utafikiri Farao,” alisema Mchungaji Lusekelo.
Mchungaji huyo anayefahamika zaidi kwa jina la Mzee wa Upako, alisema kuwa viongozi hawataki kusikiliza ushauri kutoka kwa watu wengine kwa sababu wanaamini kuwa wamesoma, wana hekima, wamesafiri sana na wanaijua nchi kuliko mtu mwingine.
“Kwa hiyo tatizo limeanza baada ya wanasiasa kuweka pamba masikioni. Nchi inahitaji uwanja mpana zaidi wa mawazo ndipo unaweza kuijenga, hasa katika mfumo wa sasa wa uhuru wa habari na vyama vingi. Dunia ya sasa siyo ya mwaka 1970,” alisema na kuongeza:
“Ni busara tu, haihitaji kwenda shule, kusema kuwa sisi tunaijua nchi, nani asiyeijua nchi yake? Kwani sisi ni Wazambia? Kila mtu anaijua nchi yake katika eneo lake.
“Iwapo viongozi watalazimisha kupatikana kwa Katiba Mpya, haitakuwa na uzito, itapoteza heshima muda mfupi kwa kuwa itapingwa na wananchi.
“Kwa hiyo, mtapata hasara kubwa sana kwamba mlitumia Sh75 bilioni kwa Warioba (Jaji Joseph Warioba, Tume ya Mabadiliko ya Katiba) na bilioni kadhaa kwenye Bunge la Katiba. Atakayeumia sana Katiba Mpya ikianguka ni yule aliyeanzisha wazo. Tanzania haiwezi kuandika Katiba katika mazingira haya.”
Aliongeza kuwa katika hali ya kawaida hauwezi kuanzisha mashindano ya mbio ukiwa peke yako halafu ukajipongeza kwa kushinda.
“Au mpira uko peke yako, unafunga goli, halafu unasema ehhh nimefunga, haiwezekani,”alisema.
Kiongozi huyo, alisema kwamba anaamini Rais ajaye wa awamu ya tano, ataweza kuwaunganisha wananchi waliotofautiana kutokana na Mchakato wa Katiba kwa kuwa mazingira ya sasa hayawezi kuwapa wananchi Katiba wanayoitaka.
“Mwaka 2016 unamwacha rais wa awamu ya tano atusaidie kuirudisha nchi pamoja, tuligawanyika, unaponya majeraha halafu mwaka 2017 Bunge la Katiba linaendelea,” alisema.
Hata hivyo, alieleza kwamba kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kufanyika, Bunge la Jamhuri ya Muungano litapaswa kufanyia marekebisho baadhi ya vipengele kwenye Katiba ya sasa vinavyolalamikiwa, ambavyo ni suala la mgombea binafsi, Tume ya Uchaguzi na madaraka ya Rais.
“Rais apunguziwe madaraka kidogo kwa sababu Rais wa Tanzania ana madaraka makubwa mno, ukimtoa Mungu anakuja yeye. Bahati, Mungu ametusaidia katika vipindi vinne, tumepata marais ambao tumeishi kwa huruma zao,” alisema.
Vilevile aliwataka wanasiasa kukumbuka kuwa amani na chakula kinachopatikana nchini leo ni matokeo ya mazingira yaliyoandaliwa na viongozi miaka ya 1960 na 1970 na kwamba uamuzi wowote wanaofikia leo lazima ukusudie kulinufaisha taifa kwa miaka mingi ijayo.
“Viongozi wa sasa hivi hawataki kutengeneza mazingira ya miaka 30, 40 ijayo, hawajui jamii lazima ibadilike, sasa wakati wote mabadiliko ukiyasubiri yaje huwa yanajileta na maafa sana,” alieleza.
Joto la uchaguzi
Akizungumzia kuhusu joto la kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais mwaka 2015, Mzee wa Upako alisema unatarajiwa kuwa mgumu kwa kuwa tayari watu wenye majina makubwa wameshaanza kuonyesha nia ya kuwania nafasi hiyo ya juu nchini.
“Ingekuwa nafuu kama rais huyu anaendelea, lakini tunabadilisha rais na ukisoma hisia, unaona wanaogombea urais hata ndani ya CCM ni wakubwa, siyo watu wadogo, wana makundi makubwa kwenye chama chao,” alisema.
Alibainisha kuwa kutokana na mchakato wa urais kuanza chini kwa chini, baadhi ya wananchi na viongozi wameanza kugawanyika kila mtu akimtaka rais atakayenufaika naye.
Pia, alisema katika uchaguzi huo, siyo vyema kupuuza nguvu ya vyama vya upinzani kwa kuwa vina wafuasi wengi baadhi ya maeneo nchini.
“Unaweza kupuuza nguvu ya Chadema, NCCR-Mageuzi na CUF huku Tanzania Bara, lakini huwezi kupuuza nguvu ya CUF Zanzibar. Wabunge wote wa CUF na wawakilishi wao hawapo kwenye Bunge la Katiba, ukitoa Hamad Rashid hawako wote. Nguvu ya kisiasa Zanzibar kati ya CUF na CCM ni asilimia moja kwa 49,” alisema.
Sifa za Rais ajaye; vijana wakae kando
Akizungumzia kuhusu sifa za rais ajaye, alisema hata ikitokea kijana mwenye miaka 45 akiingia katika kinyang’anyiro hicho, hawezi kupata nafasi kwa kuwa umri huo hautoshi kulifahamu taifa vizuri.
“Naamini katika umri, unaweza kusema Mwalimu Julius Nyerere alikuwa na miaka 38 alipokuwa Waziri Mkuu, hayo yalikuwa ni mazingira ya wakati ule, lakini siyo kama leo,” alisema na kuongeza:
“Rais anatakiwa kuanzia miaka 50 na kuendelea, huo ndio ukweli hata kama watasema urais ni taasisi kwa miaka 40 umeijua nchi wapi? Hata akina Nyerere (Julius Nyerere) iliwasumbua sana.”
Alizitaja sifa nyingine kuwa ni pamoja na kujua matatizo ya Watanzania ukiwamo umaskini, uzalendo, mwadilifu ambaye hana kashfa, siyo mdini wala mdhehebu, rais ambaye ataendelea kuwaunganisha Watanzania na atakayesimamia Katiba ya nchi.
“Sijajua Katiba ya sasa itaitamkaje Zanzibar, tupate watu wanaosimamia Katiba, sasa unaona Katiba ya Zanzibar imevunja Katiba ya Jamhuri wa Muungano. Tunataka rais wa awamu ya tano ambaye ni jasiri, ukicheza na matendo yanayoshiria uvunjifu wa amani rais anakuwa mkali kwa wahalifu,” alisema.
Kuhusu baadhi ya watu wanaotajwa kutaka kugombea urais, alisema baadhi yao wana sifa alizozitaja isipokuwa wale ambao walishakuwa kwenye madaraka wakashindwa kuleta maendeleo.
“Sasa wewe serikalini ulisahau nini? Ulikaa pale miaka yote, chochote haujaonyesha, sasa unataka kurudi tena kwa njia nyingine, haiwezekani. Hauwezi kupata mabadiliko kwa kutumia watu walewale kwa njia zilezile, kwa hiyo lazima upate watu ambao hawajawahi kushika madaraka makubwa ya nchi au walishika madaraka makubwa walionyesha utendaji.”
Kuhusu maadili ya viongozi wa umma
Mzee wa Upako alisema ingawa hakuna kipimo cha mtu aliyejilimbikizia mali, viongozi wanaofanya hivyo ni wale yenye hofu na wasio na uhakika na maisha yao baada ya kustaafu.
“Sisi hatukatai mtu kuwa na mali, lakini apate katika njia iliyokuwa halali. Haumizi wenzake na kuliingiza taifa kwenye mikataba isiyo na tija. Binadamu anastahili kula, hastahili kuwa mlafi, anastahili kuwa na mali, lakini siyo mali iliyopitiliza katikati ya watu maskini,” alisema.
Akitoa mfano namna maisha ya viongozi wa umma na watoto wao yalivyokuwa miaka ya 1970, alisema: “Mimi nimesoma na watoto wa Mkuu wa Mkoa Mwakabongo, wadogo zake Waziri Mwakawago, watoto wa Makweta shule moja. Wote tulikuwa tunavaa makobazi.”
Alisema hali ni tofauti hivi sasa, ambapo kuna shule za maskini na matajiri. Viongozi waliojilimbikizia mali ni vizuri wakaifikiria zaidi jamii, maana ikisambaratika hata mali yao haitakuwa na thamani.
“Hata ukikimbilia Ulaya kunakuwa kuzuri tu kama nyumbani kuna amani. Nasema wenzetu wenye dhamana wafanye jitihada kulitoa taifa kwenye umaskini.”
Vitega uchumi na amani nchini
Mzee wa Upako, alisema kuwa baada ya miaka 10 Tanzania haipaswi kuwa katika hali ya kiuchumi iliyonayo sasa na kwamba kama hakutakuwa na mabadiliko, amani itatoweka nchini.
“Kama nchi hii itakuwa maskini hivi kwa miaka 10 ijayo usitegemee itakuwa kisiwa cha amani tena. Huku chini kumeshaanza kuteketea, ukipata ajali hapa watu hawakimbilii kukuokoa wanakimbilia kukusachi. Viashiria vimeshaanza kuonyesha kwamba watu wanaendekeza njaa, kuliko utu wao.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment