Writen by 
                            sadataley
6:14 PM
                            - 
                            
0
                            Comments
                          
 
  
            
“Ni muhimu  kudumisha amani nchini, tusizipe nafasi tofauti zetu za 
kidini kwani tusipokuwa waangalifu tunaweza kusababisha mvurugano katika
 jamii yetu”
Alhad Mussa Salum 
            
Na Waandishi Wetu, MwananchiDar na Mikoani. Karibu katika kila mkusanyiko 
wa swala ya Idd el Fitri, neno “Katiba” lilitajwa wakati viongozi wa 
dini ya Kiislamu walipokuwa wakitoa mawaidha yao ya sikukuu hiyo 
kusherehekea kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Mfungo wa Ramadhani.
Katika mahubiri hayo, viongozi hao wa kidini walitaka mchakato wa Katiba uzingatie masilahi ya umma.
Mahubiri hayo yamekuja zikiwa zimebaki siku saba 
kabla ya vikao vya Bunge Maalumu la Katiba kuendelea mjini Dodoma, 
lakini kukiwa na sintofahamu kutokana na wajumbe wanaounda Kundi la 
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao kwa madai ya 
kutozingatiwa kwa maoni yaliyotolewa na wananchi.
Ukawa wanadai mjadala wa Katiba ni lazima ujikite 
kwenye Rasimu ya Katiba, ambayo imebeba mapendekezo ya wananchi na hali 
kadhalika kutaka wajumbe wenzao, hasa kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) 
kuacha kujenga hoja kwa kutumia kejeli, matusi na mizaha.
Jijini Dar es Salaam, Baraza Kuu la Waislamu 
Tanzania (Bakwata), liliisihi Ukawa kurudi bungeni ili kuweza 
kukamilisha mchakato wa kupata Katiba Mpya, lakini likasema mjadala huo 
uzingatie Rasimu ya Katiba.
Katika salamu zake za Idd, Katibu Mkuu wa Bakwata,
 Alhaji Suleiman Lolila alisema tayari fedha nyingi za umma 
zimeshatumika kuandaa mchakato wa Katiba Mpya, hivyo siyo busara kususia
 mchakato wake katika hatua zake za mwisho.
“Baraza linawasihi waliosusia warejee bungeni kwa 
sababu gharama kubwa zimeshatumika na kama kuna tofauti ziende 
zikajadiliwe na kumalizwa ndani ya Bunge,” alisema Lolilo.
Aliongeza kuwa Baraza linasikitika kwani maoni ya 
Waislamu hayakutiliwa maanani katika kuandaa Rasimu ya Katiba Mpya na 
kwamba wanaamini yatazingatiwa katika hatua zinazofuata za mchakato huo.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akihutubia Baraza la Idd
 jijini Dar es Salaam, alisema  mchakato wa Katiba Mpya una lengo zuri 
kwa masilahi ya taifa na katika mtikisiko ambao wamepitia hadi sasa ni 
vyema ukafikia mwisho na maelewano yapatikane.
“Walioko nje ya Bunge nawaomba warudi ndani kwani 
huko ndiko tunakoweza kujadiliana, tukatofautiana na kufikia hatua 
kufika makubaliano na nashukuru hata viongozi wa dini mmeligusia hilo,” 
alisema Pinda.
Alieleza kwamba kwa sasa kilio cha Watanzania 
wengi ni kuona Bunge la Katiba likiendelea kwa wale walio nje kurudi 
ndani kisha kujitazama upya na kupitia kuhusu udhaifu wote wa Katiba ya 
zamani na kurekebisha kwa ajili ya kupata Katiba nzuri itakayotupeleka 
mbele kwa miaka mingine mingi ijayo.
Naibu Kadhi, Masheikh 
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/Katiba/-/1625946/2402444/-/xy19wtz/-/index.html
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/Katiba/-/1625946/2402444/-/xy19wtz/-/index.html
 
 
 
 
 
 
 
No comments
Post a Comment