Writen by
sadataley
6:14 PM
-
0
Comments
Na Waandishi Wetu, MwananchiDar na Mikoani. Karibu katika kila mkusanyiko wa swala ya Idd el Fitri, neno “Katiba” lilitajwa wakati viongozi wa dini ya Kiislamu walipokuwa wakitoa mawaidha yao ya sikukuu hiyo kusherehekea kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Mfungo wa Ramadhani.
Katika mahubiri hayo, viongozi hao wa kidini walitaka mchakato wa Katiba uzingatie masilahi ya umma.
Mahubiri hayo yamekuja zikiwa zimebaki siku saba
kabla ya vikao vya Bunge Maalumu la Katiba kuendelea mjini Dodoma,
lakini kukiwa na sintofahamu kutokana na wajumbe wanaounda Kundi la
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao kwa madai ya
kutozingatiwa kwa maoni yaliyotolewa na wananchi.
Ukawa wanadai mjadala wa Katiba ni lazima ujikite
kwenye Rasimu ya Katiba, ambayo imebeba mapendekezo ya wananchi na hali
kadhalika kutaka wajumbe wenzao, hasa kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM)
kuacha kujenga hoja kwa kutumia kejeli, matusi na mizaha.
Jijini Dar es Salaam, Baraza Kuu la Waislamu
Tanzania (Bakwata), liliisihi Ukawa kurudi bungeni ili kuweza
kukamilisha mchakato wa kupata Katiba Mpya, lakini likasema mjadala huo
uzingatie Rasimu ya Katiba.
Katika salamu zake za Idd, Katibu Mkuu wa Bakwata,
Alhaji Suleiman Lolila alisema tayari fedha nyingi za umma
zimeshatumika kuandaa mchakato wa Katiba Mpya, hivyo siyo busara kususia
mchakato wake katika hatua zake za mwisho.
“Baraza linawasihi waliosusia warejee bungeni kwa
sababu gharama kubwa zimeshatumika na kama kuna tofauti ziende
zikajadiliwe na kumalizwa ndani ya Bunge,” alisema Lolilo.
Aliongeza kuwa Baraza linasikitika kwani maoni ya
Waislamu hayakutiliwa maanani katika kuandaa Rasimu ya Katiba Mpya na
kwamba wanaamini yatazingatiwa katika hatua zinazofuata za mchakato huo.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akihutubia Baraza la Idd
jijini Dar es Salaam, alisema mchakato wa Katiba Mpya una lengo zuri
kwa masilahi ya taifa na katika mtikisiko ambao wamepitia hadi sasa ni
vyema ukafikia mwisho na maelewano yapatikane.
“Walioko nje ya Bunge nawaomba warudi ndani kwani
huko ndiko tunakoweza kujadiliana, tukatofautiana na kufikia hatua
kufika makubaliano na nashukuru hata viongozi wa dini mmeligusia hilo,”
alisema Pinda.
Alieleza kwamba kwa sasa kilio cha Watanzania
wengi ni kuona Bunge la Katiba likiendelea kwa wale walio nje kurudi
ndani kisha kujitazama upya na kupitia kuhusu udhaifu wote wa Katiba ya
zamani na kurekebisha kwa ajili ya kupata Katiba nzuri itakayotupeleka
mbele kwa miaka mingine mingi ijayo.
Naibu Kadhi, Masheikh
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/Katiba/-/1625946/2402444/-/xy19wtz/-/index.html
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/Katiba/-/1625946/2402444/-/xy19wtz/-/index.html
No comments
Post a Comment