Writen by 
                            sadataley
6:35 PM
                            - 
                            
0
                            Comments
                          
                  
  
  

Jeshi la Nigeria limepiga marufuku utumizi wa magari katika jimbo la Borno
Jeshi la Nigeria limepiga 
marufuku utumizi wa magari kwa siku tatu katika jimbo la Borno kaskazini
 mashariki mwa taifa hilo ili kuzuia tishio la wanamgambo wa Boko Haram.
Msemaji wa jeshi amesema kuwa hatua hiyo itazuia
 utumiaji wa magari kutekeleza mashambulizi ya kujitolea mhanga wakati 
wa siku kuu ya Eid ul Fitr.Wakati huohuo kumekuwa na ripoti ambapo mlipuaji wa kujitolea muhanga amewaua watu kadhaa katika mji wa kazkazini wa KANO.

Kundi la Boko Haram limetishia kulipua bomu la gari
Gavana wa Borno Kassim Shetima amesema kuwa anawaonea huruma maelfu ya watu waliolazimika kutumia mda wao mwingi kutembea hadi katika viwanja vya kufanyia salah,lakini akaongezea kuwa hatua hiyo inalenga kuwalinda .

Jeshi la Nigeria limepiga marufuku utumizi wa magari katika jimbo la Borno
Jeshi la Nigeria hivi majuzi lilikiri kwamba baadhi ya wanajeshi wake walikuwa wanatoroka kutokana na uvamizi wa wanamgambo hao.
 
 
 
 
 
 
 
No comments
Post a Comment