Sunday, June 30, 2013
KUELEKEA KOMBE LA DUNIA NA MAANDAMANO HUKO BRAZIL
Rais wa Fifa Sepp Blatter, anaamini kuwa hadhi ya shirikisho la mchezo wa soka duniani imeimarika kutokana na fainali za kombe la shirikisho, inayoendelea nchini Brazil, licha ya maandamano yanayoendelea nchini humo.
Maandamano yanayoendelea nchini Brazil
Akiongea kwa mara ya kwanza, tangu maandamano hayo kuanza, Blatter amesema anawahurumia raia wa nchi hiyo wanaoandamana katika miji mia moja nchini Brazil.
Maandamano zaidi yanatarajiwa kabla ya fainali za kombe hilo siku ya Jumapili kati ya Brazil na Uhispania katika uwanja wa Marikani mjini Rio.
Kuna wasi wasi mkubwa kuwa huenda rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff huenda asihudhuria fainali hiyo.
'' Fifa imekuwa na nguvu zaidi na hadhi yetu imeimarishwa. Mchezo wa soka umekuwa na nafasi kubwa miongoni mwa taifa hili na imewapa fursa ya kuelezea hisia zao'' Alisema Blatter.
Blatter amesema anawahurumia sana raia wa nchi hiyo kwa kuwa anafahamu masuala wanayoyapinga kupitia maandamano hayo ya amani na ameongea kuwa anatarajiwa serikali ya nchi hiyo itatatua masuala hayo kabla ya kuanza kwa fainali ya kombe la dunia itakayoandaliwa nchini humo mwaka ujao.
Shirikisho la mchezo wa FIFA limeshutumiwa sana nchini Brazil kwa kupata faida kubwa isiyotozwa ushuru kutokana na fainali za kombe la dunia kuandaliwa nchini humo, na kuiacha taifa hilo kuwekeza mabilioni ya fedha za umma bila manufaa yoyote. Bwana Blatter hata hivyo amekanusha madai hayo.
''Dhamira kuu ya kombe la dunia sio kupata faida au kuchukua faida yote kutoka kwa nchi inayoandaa mashindano hayo, lakini ni kuisaidia taifa hilo ili kuhakikisha kuwa fainali hizo zinafanikiwa'' Alisema Blatter.
Blatter ambaye aliondoka nchini Brazil wiki iliyopita, huku maandamano hayo yakichacha, amepuuzilia mbali madai kuwa alitoroka Brazil hata bila kuwajulisha maafisa wengine wakuu wa Fifa.
Blatter amesema aliondoka Brazil ili kuhudhuria fainali za kombe la dunia kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 inayoandaliwa nchini Uturuki.
Kiongozi wa Al Shabaab ajisalimisha
Hassa Dahir
Mmoja wa viongozi wakuu wa zamani wa kundi la wapiganaji wa Al-shabaab, Hassa Dahir Aweyes amewasili mjini Mogadishu chini ya ulinzi mkali wa vikosi vya serikali.
Hata hivyo haijulikani iwapo kiongozi huyo amesalimu amri au ameamua kujiunga na vikosi hivyo vya serikali.
Ijumaa iliopita, umoja wa mataifa ulitangaza kuwa Bwana Hassa Dahir alikuwa amejisalimisha kwa vikosi vya serikali ya Somali lakini madai hayo yakapingwa na wazee wa koo za taifa hilo.
Kiongozi huyo alikuwa amechukua hifadhi katika mji wa Kazkazini wa Adado baada ya makabiliano makali kuzuka kati ya kambi tofauti za wapiganaji wa Al Shabaab juma lililopita.
Kiongozi huyo ametajwa kama gaidi na umoja wa mataifa pamoja na serikali ya marekani.
MZUNGU AKISAKATA MUZIKI WA INJILI WAKATI WA MAADHIMISHO YA MIAKA MITATU YA KTUO CHA REDIO CHA KKKT- DAYOSISI YA IRINGA
RADIO FURAHA 96.7FM JANA
HUYU NI MMOJA WA MARAFIKI WAKUBWA WA RADIO FURAHA
KWELI KANISA LITAENDELEA KUWEPO DAIMA
"YESU ANAUTAJIRI MKUBWA SANA"
Leo hii ni kilele cha Sikukuu ya Vijana kwa Usharika wa Kihesa Dayosisi ya Iringa (KKKT) hapa utaona ni sura za vijana, leo vijana walipewa nafasi kuonesha kama kweli wanaweza kutumika katika shamba la Bwana wetu Yesu Kristo. Kutoka kushoto ni James Gasso, Ohard Mpesa, Happy Mdegella,Odiana Ngasakwa na mwisho ni Eliud Nduye na nyuma yao ni Mchungaji kijana kabisa Mchungaji Kurwa Sadataley
KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA
DAYOSISI YA IRINGA
SIKUKUU YA VIJANA USHARIKA WA KIHESA
JIMBO LA KASKAZINI
NENO KUU : VIJANA NI KIU YA MABADILIKO KATIKA JAMII
"SOTE TUKUBALI KUTUMWA KATIKA JAMII KWA HUDUMA MBALIMBALI TUNAZOITWA NA TULIZOITWA"-ISAYA 6:1-7
Katikati ni Mkuu wa Jimbo la Kaskazini Mchg. Donald Kiwanga, kushoto ni Mchg. Yusto Kinyoa na Mchg. Kisabugo
Wazee wa kanisa wakiwa kazini
Mkuu wa Jimbo akizungumza na vijana baada ya ibada ya Pili leo hii hapa katika Usharika wa Kihesa
Mchg. Yusto Kinyoa na Mchg. Kisabugo mara baada ya Ibada ya pili
Wazee wa Kanisa Vijana wakiwa na Wachungaji
Wazee wa Kanisa wakiwa na Mchungaji Kijana Mchg. Kurwa Sadataley
Sumaye: Vijana msikubali kununuliwa kwenye Uchaguzi
Na Pamela Chilongola na Benjamin Mwangoka, MwananchiDar es Salaam. Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amewatahadharisha vijana kuwa wanaelekea kwenye uchaguzi mkuu wasikubali kupewa rushwa ya kanga, fulana na fedha na mtu yeyote anayetaka kuingia madarakani.
Akizungumza jana alipokuwa kwenye bonanza la michezo la kikundi cha Ukwamani Jogging kilichopo Kawe, alisema vijana wawe makini katika kuchagua mtu mwenye uwezo wa kuongoza ambaye atajali masilahi ya wananchi wake siyo kwa masilahi yake binafsi.
“Najiuliza kama ninajiamini nataka kugombea Kawe au Arusha au Sumbawanga kama ninafaa na wananchi wananiamini mimi ninafaa na wananchi wananihitaji kwa nini niwachochee kwa kanga au fedha ukiona hivyo huyo hawafai kuwaongoza,” alisema na kuongeza:
“Ukiona mtu anatoa kitu ili achaguliwe hafai kuwa kiongozi kwani uongozi ni mzigo,” alisema Sumaye.
Aliwashangaa watu wazima wanaochukua fedha na kuweka mfukoni kisha wanapita mitaani huku wakisema fulani anafaa kwa kuwa anatoa rushwa na fulani hafai kwa kuwa hatoi kitu chochote.
Sumaye alisema anayetoa fedha ili apewe kura huyo hafai kuwa kiongozi kwa sababu atakuwa anawatumikia watu wake waliompa fedha sio mwananchi ambaye alijitolea kumchagua kiongozi hiyo kwa kumpigia kula halali ili aweze kusaidia kumtatulia kero mbalimbali zinazomkabili.
Alisema kama kuna watu wanaumizwa kwa kuambiwa wanapokea au kutoa rushwa huku akiwa anaendelea na kufanya hivyo aache ili asiendelee kuumizwa na hilo.
Sumaye alisema nchi haiwezi kuwa na maendeleo kama viongozi wataendelea kudidimiza nchi kwa rushwa,ufisadi na kuingiza dawa za kulevya nchini.
Alisema viongozi wanaoleta dawa za kulevya kama ni nzuri wangezitumia lakini hawazitumii matokeo yake wanaoathirika ni vijana ambao wanategemewa kulijenga taifa hili.
“Hatuwezi kudidimiza jamii kwa kuwaletea dawa za kulevya ili watoto wa wenzao waharibikiwe kwa nini wasiwape au kutumia hao viongozi ili waathirike wao wenyewe?” alisema Sumaye
Saturday, June 29, 2013
Obama akutana na rais Zuma
Rais wa Marekani Barack Obama, amesema uvumilivu na ujasiri wa Nelson Mandela ni mfano mwema kwa dunia na upendo wa dhati wa rais huyo wa zamani wa taifa la Afrika Kusini inaonyesha ni kwa namna gani alivyo na utu wa kibinadamu.
Bwana Obama ameongeza kuwa Mandela, alionyesha ukweli na ukakamavu ambao una maana kubwa katika utu wa kibinadamu ambao uliondoa tabaka la ubaguzi, udini na utaifa.
Rais huyo wa marekani ameyazungumza hayo mjini Pretoria baada ya mazungumzo na rais wa sasa wa Afrika kusini, Jacob Zuma.
Ziara hiyo ya bwana Obama ina lengo la kuongeza mauhusiano ya kibiashara lakini imetekwa na hisia za ugonjwa wa bwana Mandela ambaye amelazwa hospitalini kwa muda wiki tatu sasa kutokana na maradhi ya mapafu yanayosumbua mfumo wake wa kupumulia.
Katika kikao hicho wawili hao walizungumza na vyombo vya habari kuhusu ushirikiano wa mataifa yao kibiashara mbali na kutafuta suluhu ya kudumu katika mataifa yaliokumbwa na ghasia mashariki ya kati.
Ikulu ya White House imesema kuwa Obama pia atakutana na familia ya Mandela anayeugua maambukizi ya mapafu ili kuifariji.
Awali Rais Obama, aliye ziarani barani afrika alitoa shukran za dhati kwa uongozi ulioonyeshwa na Mandela.
Wakati wa ziara hiyo Obama pia atakutana na wanafunzi huko Soweto kabla ya kuelekea katika jela la Robben Island ambayo Mandela alihudumia kifungo chake cha miaka 27 wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi.
KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA
DAYOSISI YA IRINGA
YAFANYA SEMINA ZA VIJANA KAMA SEHEMU YA KUSHEREHEKEA SIKUUU ZA VIJANA
HAPA NI LEO HII KATIKA USHARIKA WA KIHESA JIMBO LA KASKAZINI
IMEFANYIKA KATIKA KITUO CHA VIJANA HAPA USHARIKANI
PICHA YA SEHEMU YA KANISA NA HAPA NI MWINJILISTI NESIA MWILAFI WA USHARIKA WA KIHESA
VIJANA WAKIWA DARASANI
MKUU WA JIMBO MCHUNGAJI DONALD KIWANGA AKIFUNDISHA VIJANA
MWINJILISTI SHEM MSITE KATIBU WA VIJANA USHARIKA
HAPA WAKIWA KATIKA MAANDALIZI YA IBADA YA KESHO
KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA
DAYOSISI YA IRINGA
"NAFASI YA KIJANA KATIKA KANISA".
SOMO LILOTOLEWA KATIKA KONGAMANO LA VIJANA KATIKA USHARIKA WA KIHESA 29-06-2013
Kanisa ni nini?
Kanisa si jengo tu bali ni wale waliomo ndani yake. Maana yake ya asili toka neno la Kiyunani ni ekklesia “kusanyiko” "walioitwa" kama maneno katika msalaba ambao huwa ninauvaa. Neno Kanisa Iimo katika Biblia, Matendo ya mitume 17:24 "Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo yeye kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono."
Kanisa si jengo tu bali ni wale waliomo ndani yake. Maana yake ya asili toka neno la Kiyunani ni ekklesia “kusanyiko” "walioitwa" kama maneno katika msalaba ambao huwa ninauvaa. Neno Kanisa Iimo katika Biblia, Matendo ya mitume 17:24 "Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo yeye kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono."
Kanisa ni watu wanao amini Waefeso
2:21 "Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe
hekalu takatifu katika bwana." 1Wakorintho 3:16 "Hamjui ya kuwa ninyi
mmekuwa hekalu la Mungu na yakuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?.
Kazi ya kanisa ni ipi? Kanisa linaeneza
ijili 2 Timotheo 4:2 "Lihubiri neno
uwe tayari wakati ufaao na wakati usiokufaa karipia kemea na kuonya kwa
uvumilivu wote na mafundisho."
Kanisa limepewa maagizo na Mungu
Waefeso 4:12 "Kwa kusudi kuwakamilisha watakatifu hata kazi ya huduma
itendeke hata mwili wa Kristo ujengwe."
Kila mshiriki ana jukumu maalum 1
Wakorintho 12:13, "Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa
mwili mmoja kwamba tu wayahudi au kwamba tu wayunani ikawa tu watumwa au ukawa
tu huru nasi tulinyweshwa Roho mmoja."
Wakristo tu wafariji wenzetu Waebrania
10:25 "Wala tusiache kukusanyika pamoja kama ilivyo desturi ya wengine;
bali tuonyane na kuzidi kufanya hivyo kwa kadiri muonavyo siku ile kuwa
inakaribia.
Hivyo naenda kusema kuwa ndiyo sababu siku zote nikijitazama
kama kijana humuona Mungu kuwa ni wa ajabu kuniumba hata mimi na kunifanya kuwa
Mchungaji. Hivyo hukubaliana na nyimbo na waimbaji hawa ambao wamewahi sema
kupitia nyimbo zao kuwa
a.
“Mungu wetu ndiye Boma”- Tumwabudu Mungu Wetu 302 na Dr. Martin
Luther
Mungu ndiye ngao yetu na siraha yetu shetani akija kwetu tukiwa
naye daima tutashinda na maadui zetu (shida,adha na changamoto za maisha
yetu yote). Tumtazame yeye kama Dr.
Martin Luther alivyosema katika maneno ya wimbo wake huu. Anaimba wakati akiwa
katikati ya mapambano na sisi tuimbe tunapopita katika hali mbalimbali katika
maisha yetu.
b.
“Mungu ni Mwaminifu”. -Solomon Mkubwa
Mungu hatotuacha daima yeye hutunza maagano(makubaliano yetu
nay eye) hivyo hata sisi tulivyo hapa anatujua na anaendelea kutunza uaminifu
wake kwetu hivyo na sisi tusimame kwake tu, tumtazame yeye pekee.
c.
“Liseme kwani ni jambo usilolijua”- Sarah K
kwani ni hakika hatuna tunalolijua katika
maisha yetu ni yeye (Yesu) anatuwezesha ,ametuwezesha na ataendelea kutuwezesha.
d.
“I will be There, Just Call My
name”. -Michael
Jackson&Mariah Carey
Ipo siku tutaitwa kwenda Mbinguni na kila mmoja wetu ataitwa
kwa jina lake; hivyo tujiandae.
e.
“Heri Kumjua Yesu Bwana”. Tumwabudu Mungu Wetu 175 na F.J Crosby
Ni Yesu pekee atatuwezesha na kutuvusha na hata sasa anajua
tulikotoka,tulipo na tuendako.
f.
“Msingi wa Kanisa Ndiye Yesu Bwana”.
Tumwabudu Mungu Wetu 268 na samuel Stone
Kama tulivyoimba siku ile ya Kipaimara hebu tuendele
kumtazama yesu kama msingi wa Kanisa na ndiyo njia pekee ya kutuvusha vijana,
njooni tumtumikie kadili ya nafasi tunazojali. Tusiogope huku ni kuzuri tu
hakuna shida yoyote.
LEO HII NAKUONA KIJANA MWENZANGU KAMA:-
- MSHARIKA
MKAMILIFU ALIYEPO NA AJAYE
- KIONGOZI
WA KANISA-MZEE WA KANISA-MTUMISHI WA MUNGU KADA MBALIMBALI
- MLEZI
WA FAMILIA AJAYE NA ALIYEPO (wajibu wako pale nyumbani kwa sasa).
- MZAZI AJAYE – (unayoyafanya sasa nawe utafanyiwa na m/watoto wako).
- MTETEZI
WA WANYONGE (Haki za wanyonge na
wanaonyanyaswa kuto kaa kimya kwani Dr. Martin Luther alisema utawajibika
kwa yale uliyoyasema na usiyoyasema lakini ulipaswa kuyasema na umekaa
kimya.)
- MWANA
MAENDELEO ( Jiandae kuajili au
kuleta mabadiliko katika eneo ambalo Mungu atakupa/amekupa).
A. “Mkumbuke Muumba wako siku za
ujana wako kabla hazijaja siku zilizo mbaya…” (Mhubiri12:1)
B. “Nimewaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu,
na neno la Mungu linakaa ndani yenu,
nanyi mmemshinda yule mwovu”.
(I Yohana 2:14b).
C. “Na nimwibie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu
katika habari za shamba lake la mzabibu. Mpenzi wangu alikuwa na shamba la
mizabibu,kilimani penye kuzaa sana;akafanya handaki kulizunguka pande zote,
akatwaa mawe yake,akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri, akajenga mnara
katikati yake, akachimba shinikizo ndani yake;akatumaini ya kuwa utazaa zabibu,
nao ukazaa zabibu-mwitu. Na sasa, enyi wenyeji wa yerusalem, namyi watu wa Yuda
amueni, nawasihi mkato, kati ya mimi na shamba
langu la mizabibu….”(Isaya 5:1-7).
UELEWA JUU YA UJANA NA KIJANA
1.
Ujana
ni hatua ambayo mtu anaipitia baada ya utoto au ni kipindi cha kati cha makuzi
ya mtu kabla ya utu uzima na hatimae uzee
2.
Ujana
huanza mara baada ya mtu kubadilika kimaubile na huanzia miaka kumi na mbili
wengine hadi kumi na tano ambapo mtu huanza kuwa na hisia za kimwili na
kutamani sana kuwa na uhuru wake katika maamuzi. Mabadiliko haya huchochea au
hupelekea hisia mbalimbali za kimwili na mabadiliko ya jumla ya tabia
3.
Ujana
ni majira yanayopita katika makuzi ya mwanadu, ukifanikiwa kuwa mzee ni lazima
ulipita katika kipindi hiki au daraja hili la ujana, kwa hiyo kama bado uko
katika dara hili ni muhimu kujipanga ili usije ukajilaumu mbele ya safari
ZINGATIA HII
“Huwezi kuyajali maisha yako kama
hujui thamani yake, huwezi kujua thamani ya maisha yako kama hujajitambua kwa
Neno la Mungu, huwezi kuwa na maisha ya mafanikio kama maamuzi yako
hayatengenezi mafanikio, ufahamu sahihi juu ya maisha yako ndio msingi wa
kujitambua kwako, yaani kuijua Kweli ili hiyo Kweli ikuweke huru na ndipo
utakapokuwa huru kweli kweli, kumbuka hata usipoamua maisha yako yataendelea
kama kawaida. Zaidi ya hayo kama hujui wewe ni nani huwezi kujua thamani yako,
kama hujui thamani yako lazima utaishi chini ya kiwango cha maisha unayotakiwa
kuishi”.
UTAIJUAJE NAFASI YAKO KAMA KIJANA
Nafasi yako kama Kijana ni wajibu
wako, umuhimu ulionao kwako na kwa jamii kwa ujumla wake pamoja na familia
yako. Lazima ujue nafasi yako katika maeneo yafuatayo:
• Kwako binafsi,
• Katika familia yako,
• Kwa Kanisa lako,
• Kwa jamii yako
• kwa mkoa wako,
• kwa Taifa lako na
• kwa Ufalme wa Mungu.
Safari ya kujua nafasi yako katika
maeneo yako hayo hayo hapo juu inaanzia katika eneo moja tu ambalo ni KUJITAMBUA
KUJITAMBUA NI NINI
“Kujitambua ni hali ya kuwa na
ufahamu au uelewa (kujua) wa kutosha juu ya maisha yako kwa ujumla pamoja na
mazingira yanayokuzunguka na hivyo kukufanya uishi maisha yanayofanana au
kulingana na kusudi la Mungu kwako, uishi katika ubora wa maisha yanayolingana
na kiwango cha ufahamu ulionao au kiwango cha kujitambua kwako kutegemeana na
nguvu ya taarifa unazopata.
HIVYO BASI KIJANA ANATAKIWA
KUJUA KUWA:-
1. Kujitambua ni hatua ya muhimu
katika maisha ya mtu yoyote duniani kama anataka kuishi kwa Furaha na matumaini
na kufikia malengo yake
2. Kujitambua ni matokeo ya kupata
ufahamu sahihi juu eneo fulani utakaokusaidia kufanya maamuzi sahihi katika
eneo husika ili uweze kufanikiwa
3. Ufahamu au maarifa unapatikana
kwa kutafuta, kuchunguza na kudadisi taarifa mbalimbali kwani si kila namna ya
kujitambua ni sahihi kwa kijana
4. Matokeo ya ufahamu ulionao
yatafanana na ubora wa maisha unayoishi kwa kiwango cha kuathiri maamuzi yako
ya kila siku
5. Kiwango cha matokeo ya kujitambua
kitafanana na ubora wa taarifa ulizozipata
6. Udhihirisho wa maisha ya
kujitambau ni hatua ya juu kabisa ya kuthibitisha kwamba kweli umejitambua.
KUJITAMBUA NI LAZIMA KWANI:-
1. Ni lazima ujitambue, upate
ufahamu sahihi juu ya maisha yako pamoja na mambo yote na jamii inayokuzunguka
2. Ni muhimu ujue wajibu ulionao
kwako wewe mwenyewe kama mtu binafsi juu ya maisha yako
3. Kuna haja ya kujua kuwa wewe ni
sehemu ya familia yako na lazima ujue wajibu wako kwa wazazi na familia kwa
ujumla
4. Ni lazima ujifunze kuwa mzalendo
wa taifa lako sawa na jinsi ambavyo Mungu anataka, fahamu kuwa umeunganishwa na
ardhi ya Tanzania kwa mafanikio yako, Mungu akikwambia nenda nje ya nchi nenda
lakini usifikiri mafanikio hayako Tanzania
5. Kijana unatakiwa ujitambue, ujielewe kuwa wewe ni nani na una kusudi gani katika maisha yako
6. Unatakiwa kupata uelewa wa
kutosha juu ya kipindi cha ujana na umuhimu wake ukiwa bado Kijana ili ujue
namna ya kuzingatia na kujipanga kwa hapo baadae
7. Kuelewa changamoto zilizopo
katika kipindi cha ujana na namna ya kuzishinda kuna uhusiano na namna
unavyojitambua ukiwa bado kijana
8. Kujenga shauku, nia na kiu kwa
kijana ili aweze kuishi maisha yenye mwelekeo na aweze kutimiza maono yake
akiwasaidia na wengine kumjua Mungu na maisha yake kwa ujumla wake
9. Kuwekeza uthamani na nguvu ya
kipindi cha ujana kwa mtazamo wa Ufalme wa Mungu.
Imeandaliwa na
Mchg Kurwa Sadataley- Mratibu wa
Idara
Habari na Mawasiliano KKKT-DIRA
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)
Social Buttons