Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, March 17, 2018

Kigogo wa FBI afukuzwa kazi

Kutoka nchini Marekani Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jeff Sessions amemfuta kazi aliyewahi kuwa Kaimu Mkurugenzi Mstaafu wa FBI Andrew McCabe ikiwa ni siku chache tu kabla ya kustaafu rasmi na kupata haki zake zote za mafao.

Taarifa ya Sessions imeeleza kuwa McCabe amefukuzwa kazi kutokana na kuvujisha taarifa za uongo na kuwapotosha wapelelezi. Kigogo huyo wa FBI amekataa kuhusika na tuhuma hizo.

Ameeleza kuwa amezushiwa tuhuma hizo kwasababu alihusika katika kufuatilia suala la nchi ya Urusi kuingilia Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2016.

Rais Donald Trump amewahi kumtuhumu McCabe kuwa na upendeleo wa kisiasa kwa kuwa mfuasi wa Chama cha Democrats.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment