Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, June 16, 2017

Trump kutangaza sera mpya dhidi ya Cuba

Rais wa Marekani, Donald Trump, leo anatangaza mabadiliko ya sera kuhusu Cuba ambapo anatarajiwa kuyazuwia makampuni yanayofanya biashara ya kijeshi na Cuba pamoja na kuimarisha sheria za usafiri kuelekea kisiwa hicho.

Kuba - Tourismus - USA (picture alliance/EFA/O. Barria)
Hayo yatakuwa ni kubadili sera ya kujongeleana kati ya Marekani na Cuba ilioanzishwa na Rais Barack Obama mnamo miaka ya mwisho kabla ya kuondoka madarakani.
Rasimu ya mipango hiyo ya rais iliyotolewa jana jioni na Ikulu ya Marekani imeeleza kuwa sera hizo mpya zimeandaliwa kwa ajili ya kuwawezesha watu wa Cuba. Taarifa hiyo imeeleza kuwa sera hiyo haiwalengi watu wa Cuba, bali utawala wa Cuba na kuongeza kuwa lengo lake ni la uhuru wa kisiasa na kidini pamoja na kuheshimu haki za binaadamu.
USA PK Präsident Donald Trump nach Schießerei in Alexandria, Virginia (picture alliance/abaca/O. Douliery)
Rais Donald Trump
Rais Trump anatarajiwa kutangaza sera hizo mpya mjini Miami, ambako ni makaazi makuu ya jumuiya ya Wacuba wanaoishi uhamishoni nchini Marekani ambao wanaupinga utawala wa kisiwa chao.
Katika miaka yake ya mwisho madarakani, rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama alianzisha juhudi za kidiplomasia za kujihusisha tena na adui yake huyo wa zamani wakati wa Vita Baridi, iliyohusisha kurejesha uhusiano na kuzifungua tena balozi zake. Sera hiyo itaendeleza uhusiano wa kidiplomasia na kuyaruhusu mashirika ya ndege ya Marekani pamoja na meli kuendelea kutoa huduma zake katika kisiwa hicho.
Marekani kuzuwia fedha zake kumiminwa Cuba
Maafisa wa Marekani wamewaambia waandishi habari kwamba Trump atatangaza marufuku katika utowaji wa fedha kwa jeshi la Cuba ambalo limekuwa likijitanua ili kuisaidia sekta ya utalii pamoja tawi lake la kampuni inayohusika na biashara ya zana za kijeshi linalojulikana kama GAESA, ambayo inamiliki hoteli kubwa pamoja na maduka makubwa ya rejareja na makampuni ya kukodisha magari nchini humo. Inakadiriwa kuwa kampuni ya GAESA inachangia zaidi ya nusu ya mapato yanayotokana na biashara nchini Cuba.
Kulingana na sera hizo mpya, Rais Trump pia anatarajiwa kutangaza vikwazo vikali zaidi dhidi ya Wamarekani wanaosafiri kwenda nchini Cuba. Raia wa Marekani bado wataendelea kutumia ndege za kibiashara kwenda Cuba, lakini ikiwa wana sababu 12 tu muhimu, kuanzia shughuli za uwandishi wa habari na elimu, ambazo zitawekewa masharti zaidi pamoja na kupitia makundi yaliyotambuliwa.
Kuba - Tourismus - USA (picture alliance/EFE/A. Ernesto)
Watalii wakiwa Havana, Cuba
Jan Erik ni mmoja wa watalii wa Marekani, ''naam natumaini kutokana na uzoefu wangu nchini Cuba, kwamba tutaendelea kuwa na fursa ya kusafiri duniani, ikiwa ni pamoja na Cuba. Ninaamini ni fursa kubwa sana kwa watu wanaoishi hapa kukutana na Wamarekani na kusaidia katika uchumi.''
Hata hivyo, wakosoaji wanasema kuwa mipango hiyo haitauathiri sana kiuchumi utawala wa Cuba na itakipa kisiwa hicho nafasi mpya ya kujitangaza kuwa ni mhanga wa uchokozi wa Marekani na kuwa sababu ya kuahirisha mageuzi ya kidemokrasi.
Mnamo siku ya Jumatano, Cuba ilitangaza kuwa itafanya uchaguzi wa manispaa mwezi Oktoba. Rais Raul Castro alitangaza kuwa ataachia madaraka mwezi Februari mwaka ujao, mwishoni mwa kipindi chake cha pili cha miaka mitano, lakini ameonyesha dalili kuwa ataendelea kuwa mwenyekiti wa chama  tawala cha Kikomunisti, ambacho ni chama pekee kinachoruhusiwa nchini Cuba.
DW Swahili
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment