Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 19, 2017

Mkemia Mkuu afunguka mazito

Dar es Salaam. Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria kwa wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu na wanaovunja matakwa ya sheria katika uingizaji, usafirishaji na uhifadhi wa kemikali.

Hayo yamesemwa leo na Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele wakati alipozungumza na wanahabari kuhusu kampuni ya Techno Net Scientific kukutwa na kemikali bashirifu bila usajili.

Amesema ofisi yake ilitoa usajili wa muda wa miaka miwili kwa kampuni hiyo ambao uliishia Aprili 30 mwaka 2016 lakini bado ikawa inaendelea na shughuli zake kinyume cha sheria.

Profesa Manyele alibainisha kuwa kampuni hiyo imebainika kwamba imekuwa ikiingiza kemikali nchini kwa kutumia njia za udanganyifu na vibali vya bandia.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment