Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, April 22, 2017

Mbio za magari kufanyika Iringa leo


MADEREVA 20 kutoka ndani ya nje ya nchi wanatarajia kuchuana katika mashindano ya taifa ya mbio za magari yatakayofanyika leo na kesho mkoani hapa.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Chama cha mbio za magari Iringa (IMSC), Hamid Mbatta, amewataka wananchi mkoani Iringa kutumia fursa ya mashindano hayo kukuza biashara kutokana na wageni zaidi ya 500 wanaotarajiwa kufika kushuhudia mbio hizo.

Mbatta alisema kuwa mashindano ya magari ni fursa nzuri kufanya biashara, kukuza na kuimarisha sekta ya utalii katika Kanda ya Kusini.

Alisema kuwa kuna njia tano zilizochaguliwa kwa ajili ya mashindano hayo ambayo yataanzia katika kiwanda cha maji cha Mkwawa kilichopo Iringa Mjini ambao pia ni wadhamini wakuu wa mbio hizo.

"Madereva wa Iringa watakaoshiriki ni pamoja na Ahmed Huwel ambaye anasaidiwa na Maisam Fazal, mimi Mbatta (Msaidizi wangu Sultan Chana) na mwingine aliyeomba kushiriki kupitia timu ya Mkwawa Rally ni Shanto ambaye atakuwa na msaidizi wake ni Rahim," alisema Mbatta.

Aliwataja washiriki wengine wa mbio hizo ni mkongwe Francis Mwakatundu, Gerald Miller wa Arusha na Davis Mosha wa Kilimanjaro.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka wananchi wa mkoa huo kuchukua tahadhari wakati wa mashindano ya mbio za magari huku akiongeza kuwa mbio hizo zitasaidia kutangaza Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment