Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, April 18, 2017

Madaktari bingwa wakutana kujadili fani ya upasuaji

Dar es Salaam.Wataalam wa afya katika masuala ya upasuaji wamekutana kujadili kuanzishwa kwa mpango kazi wa kitaifa utakaongalia kwa kina fani ya upasuaji.

Mkutano huo wa siku mbili umewakutanisha madaktari bingwa wa upasuaji, wataalam wa Wizara ya Afya na shirika la kimataifa la GE Foundation.

Rais wa Chama cha madaktari Bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi Profesa Andrea Pembe alisema mpango kazi huo utaweza kuweka bayana ni wataalam wangapi wanahitajika kwenye upasuaji kuwatosha watanzania wote wenye uhitaji.

Amesema mpango huo pia utaangalia ni vifaa gani vya kisasa vinahitajika sambamba na dawa bora zitakazowezesha kuwatibu wagonjwa kulingana na mazingira yaliyopo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa GE Foundation Asha Varghest alisema lengo la kutengeneza mpango huo ni kuhakikisha mpango huo unazingatia mazingira halisi ya Tanzania na kuweka njia nzuri ya namna utakavyotekelezwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment