Writen by
sadataley
12:58 PM
-
0
Comments
Jeshi la DRC FARDC katika jimbo la Kivu Kaskazini wakipiga doria mwezi Novemba 2013.
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imetangaza kusitisha ushirikiano wake wa kijeshi na Ubelgiji.
Taarifa zilizotolewa na Radio ya Umoja
wa Mataifa ya Okapi, zimesema uamuzi wa serikali ya Kinshasa unakuja
baada ya kushuhudia mvutano wa kisiasa wa chini kwa chini kati ya
serikali hizo mbili tangu kuteuliwa kwa Waziri Mkuu mpya Bruno Tshibala.
Jarida la kila wiki la Jeune Afrique
linalochapishwa nchini Ufaransa siku ya Alhamisi, msemaji wa Wizara ya
Ulinzi ya Ubelgiji Laurence Mortier, amesema amepokea taarifa hizo
kutoka Kinshasa bila maelezo yoyote.
Aidha, amesema Brussels inaendelea kufanya tathmini ya ushirikiano huo na inataka ufafanuzi zaidi kuhusu hatua hii.
Ubelgiji imekuwa ikisaidia kijeshi nchi ya DRC kwa kuwapa mafunzo wanajeshi wake miongo kadhaa sasa kuwasaidia kupambana na makundi ya waasi.
Ushirikiano huo ulianza kutiwa dosari
tangu kuanzishwa kwa Vita vya ukombozi vilivyofanikisha kuwepo utawala
mpya chini ya Marehemu rais Laurent Desire Kabila, mwaka 1996 lakini
uhusiano huu ukarejeshwa baada ya Joseph Kabila kuingia madarakani.BBC
No comments
Post a Comment