MKOA
wa Iringa umewataka wananchi na viongozi wa serikali za vijiji na
mitaa pamoja na wakuu wa wilaya zote tatu za mkoa huo kusaidia
kutekeleza agiza la waziri agizo la waziri mkuu wa jamahuri ya
muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa kwa kuwafichua wauzaji na watumiaji wa pombe kali ya viroba iliyofungashwa katika mifuko ya Plastini.
Imeelezwa
kuwa tamko la waziri mkuu la kusitisha utumiaji ,uuzaji na
ufungashaji wa pombe kali kwenye mifuko ya Plastiki maarufu kama
viroba lililotolewa Februari 16 mwaka huu utekelezaji wa maelekezo
ya tamko hilo la waziri mkuu umeanza toka Machi mosi mwaka huu
hivyo tayari mkoa umeanza oparesheni kali ya kuwasaka wale wote
wanaokiuka agizo hilo.
Akizungumza
na wanahaabari leo ofisini kwake mkuu wa mkoa wa Iringa Amina
Masenza alisema kuwa agizo hilo limekuja kufuatia athari kubwa hasa
kwa vijana na baadhi ya watoto wanaotumia pombe hiyo na kutokana na
matumizi makubwa ya pombe hiyo ambayo huuzwa bei ya chini na ubebaji
wake ni mwepesi kwa watoto wa shule na waendesha boda boda
serikali imeamua kuzuia uuzaji na utumiaji wa pombe hiyo iliyopo
kwenye Viroba .
Huku akikwepa kuyahusisha matukio yote ya ajali za boda boda kama
yanasababishwa na watumiaji wa pombe hiyo ila alisema baadhi yao
wamekuwa wakipata ajali kutokana na matumizi ya viroba na wamekuwa
wakiendesha vyombo hivyo vya moto huku wakiwa wanakunywa viroba
kutokana na pombe hiyo ni rahisi zaidi kuiweka mdomoni huku
wakiwa wanaendesha vyombo hivyo vya moto na kwa baadhi ya
wanafunzi huingia na pombe hiyo darasani bila walimu kuwaona.
Alisema
kutokana na madhara na utekelezaji wa agizo la serikali mkoa wa
Iringa umetoa maelekezo kwa wakuu wa wilaya kwa kushirikiana na
kamati za ulinzi na usalama za wilaya kufanya oparesheni ya
kudhibiti matumizi ya Viroba katika maeneo yao .
"
Pombe kali za viroba zitasakwa kuanzia kwa wasambazaji ,wanunuzi
,wauzaji wote watakaokamatwa watachukuliwa hatua kali za kisheria
...aidha kwenye vijiji kamati za ulinzi za vijiji au miotaa nazo
zimeelekezwa kufanya oparesheni ya kuthibiti matumizi ya viroba
hivyo nawaomba wananchi wote kutoa ushirikiano katika kufanikisha
udhibiti wa viroba ... Viroba ni pombe kama konyagi hivyo serikali
haijapiga marufuku matumizi ya konyagi za chupa ila imezuia pombe
hiyo iliyopo kwenye mifuko ya plastiki na pombe iliyopo kwenye
chupa ni vigumu mwendesha boda boda kuitumia huku akiendesha
usafiri huo ama mwanafunzi kuingia nayo darasani bila kuonekana"
Kuhusu
vita dhidi ya dawa ya kulevya ndani ya mkoa alisema mkoa
umefanikiwa kuwakamata watumiaji na wauzaji wa dawa za kulevya
15 kati yao wanawake ni wawili ambao watafikishwa mahakamani baada
ya upelelezi wao kukamilika huku akidai kuwa baadhi ya
wafanyabiashara wa dawa za kulevya waliotajwa kuhusika na mtandao
wa uuzaji wa dawa hizo wamekimbia mkoa na jitihada za kuwasaka
zinaendelea.
Pia
aliwataka wananchi wa mkoa wa Iringa kuendelea na vita ya
kuwafichua wale wote wanaojihusisha na matukio ya ubakaji na
kuwafichua ili kufikishwa mbele ya sheria.
Na MatukiodaimaBlog
|
No comments
Post a Comment