Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, April 1, 2016

Rwanda yataka ufafanuzi kuhusu kifo cha waziri

Jacques Bihozagara alihudumu wakati mmoja kama balozi Ubelgiji Serikali ya Rwanda imeitaka Burundi kutoa ufafanuzi kuhusu kifo cha waziri wa zamani wa Rwanda aliyefariki baada ya kuzuiliwa na Burundi kwa miezi minne akituhumiwa kufanya ujasusi. Jacques Bihozagara, aliyekuwa wakati mmoja waziri na balozi wa Rwanda, alifariki tarehe 30 Machi, muda mfupi baada ya ufikishwa katika zahanati ya gereza la Mpimba. Chanzo cha kifo chake hakijatangazwa rasmi. Mkurugenzi anayeangazia masuala ya Afrika katika wizara ya mambo ya nje ya Rwanda Eugene Ngoga, amesema: “Jacques Bihozagara ni mmoja tu kati ya Wanyarwanda wengi nchini Burundi ambao wamefariki katika hali isiyoeleweka katika kipindi cha miezi saba iliyopita. Wizara ya Mambo ya Nje ya Rwanda inataka maelezo ya ufasaha kutoka kwa watawala Burundi kuhusu hali iliyopelekea kifo cha Bw Bihozagara na ufafanuzi kuhusu sababu za kuzuiliwa kwake tangu Desemba mwaka jana”. Rwanda pia imeitaka Burundi kusaidia familia ya marehemu kusafirishwa mwili wake hadi nyumbani kwake. Balozi wa Rwanda nchini Ubelgiji alikuwa awali ameandika na kusema kifo cha Jacques kilikuwa ni "mauaji". Umoja wa Mataifa umekuwa ukiishutumu Rwanda kwa kujaribu kuipindua serikali ya Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, madai ambayo Rwanda imekuwa ikiyakanusha.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment