Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, April 4, 2016

Magufuli afuta sherehe za sikukuu ya muungano

Hii ni mara ya pili kwa Rais Magufuli kufuta sherehe za sikukuu Rais wa Tanzania John Magufuli ameahirisha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Muungano na badala yake akawataka Watanzania waiadhimishe wakiwa majumbani au wakiwa katika shughuli zao binafsi. Siku hiyo hata hivyo bado itasalia kuwa ya mapumziko kama kawaida. Agizo hilo la Dkt Magufuli aidha linaathiri shamrashamra za mwaka huu pekee. Siku hiyo huadhimishwa tarehe 26 Aprili kila mwaka kukumbuka siku sawa na hiyo mwaka 1964 ambapo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliundwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (inayojumuisha Visiwa vya Pemba na Unguja). Magufuli aamua sikukuu iwe siku ya kazi Magufuli: Vijana sharti wafanye kazi Dkt Magufuli amesema fedha ambazo zilipangwa kutumika kwa ajili ya kugharimia vinywaji, vyakula, gwaride, halaiki, burudani mbalimbali na hafla ya usiku ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni mbili za Tanzania zitumike kupanua barabara ya Mwanza Airport katika eneo linaloanzia Ghana Quarters hadi uwanja wa ndege wa Mwanza. Barabara hiyo inafanyiwa upanuzi kutatua msongamano wa mkubwa wa magari ambayo umekuwa ukiathiri shughuli eneo hilo. Dkt Magufuli amekuwa mapumzikoni nyumbani kwake eneo la Chato, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment