Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, April 10, 2016

Korea Kaskazini yaujaribu mtambo wake wa makombora

Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kufanya majaribio ya mtambo wake mpya, ambao unaweza kurusha makombora kutoka bara moja hadi jiingine, katika juhudi za kuimarisha uwezo wake wa kufanya mashambulio dhidi ya Marekani. Vyombo vya habari vya Korea Kaskazini vinasema kuwa zoezi hilo liliongozwa na kiongozi wa taifa hilo Kim Jong-un. Jaribio hilo ni katika harakati za hivi karibuni za utawala wa Pyongyang wa kuunda zana za nuklia tangu ilipofanya jaribio lake la nne la makombora ya nuklia January mwaka huu. Hatua hiyo iliiushurutisha Umoja wa Mataifa kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo vipya. Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imetoa wito kwa utawala wa Pyongyang kujiepusha na vitendo vyake vya uchochezi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment