Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, March 17, 2016

Waandamana dhidi ya uteuzi wa Lula Brazil

Raia wa Brazil nchini Sudan Kusini wamefanya maandamano katika miji kadhaa wakipinga hatua ya rais Dilma Rousseff ya kumteua mtangulizi wake Luiz Inacio Lula da Silva kama mkuu wa wafanyikazi. Katika mji mkuu wa Brasilia ,maafisa wa polisi waliwarushia waandamanaji maji yenye pilipili nje ya jumba la rais. Lula anachunguzwa katika kashfa kubwa ya ufisadi.Saa chache baada ya hatua hiyo ,jaji wa kijimbo anayeongoza uchunguzi dhidi ya Lula alitoa mawasiliano ya simu yaliorekodiwa yakionyesha kwamba bi Lula alimpatia wadhfa huo ili kumkinga dhidi ya kukamatwa. Kiongozi huyo wa Brazil ambaye yeye mwenyewe anakabiliwa na mashtaka alitetea uteuzi huo.Amesema kuwa Lula ana ujuzi mkubwa kama mpatanishi wa kisiasa ambaye atasaidi kuupiga jeki uchumi. Pia alisema kuwa rais huyo wa zamani anaweza kushtakiwa na mahakama ya juu. Sauti hiyo ya mawasiliano ilizua hisia kali katika bunge la Brazil huku kukiwa na visa vya ghasia baada ya viongozi wa upinzani kumtaka rais huyo kujiuzulu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment