Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, March 30, 2016

Trump asema hatomuunga mgombea mwengine

Mgombea aliye kifua mbele katika chama cha Republican Donald Trump ameondoa ahadi yake ya kumuunga mkono mgombea wa chama hicho iwapo hatoshinda uteuzi wa uchaguzi huo wa mwezi Novemba. Wapinzani wa bwana Trump Ted Cruz na John Kasich wamekataa kutangaza iwapo watamuunga mkono atakayeteuliwa na chama hicho. Wagombea wote wa Republican walitia sahihi kutekeleza ahadi hiyo mwezi Novemba. Ni ishara ya mwisho ya msuguano kati ya Bwana Trump na Bwana Cruz ambaye wamekuwa na mgogoro unaowahusisha wake zao. Kamati inayomuunga mkono Bwana Cruz imechapisha picha ya utupu ya mkewe Trump Melania kutoka mwaka 2000. Akimjibu, bwana Trump alituma ujumbe wa Twitter wa picha isiopendeza ya mkewe Cruz Heidi. Bwana Trump amesema kuwa amechukuliwa vibaya na viongozi wa chama cha Republican.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment