Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, March 17, 2016

Obama aongezea Korea Kaskazini vikwazo

Rais wa Marekani Barack Obama ameidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Korea Kaskazini baada ya taifa hilo kufanyia majaribio silaha za nyuklia na makombora hivi majuzi. Msemaji wa ikulu ya White House amesema Marekani na jamii ya kimataifa hawatavumilia “shughuli haramu za nyuklia” zinazotekelezwa na Korea Kaskazini. Awali, ikulu ya White House iliishutumu Korea Kaskazini ikisema inawatumia raia wa Marekani kama rahani katika juhudi za kuendeleza ajenda yake ya kisiasa. Korea Kaskazini yaamrisha majaribo zaidi ya mabomu Korea Kaskazini yajibu vikwazo vya UN Hii ni baada ya Korea Kaskazini kumhukumu mwanafunzi Mmarekani kifungo cha miaka 15 na kazi ngumu jela kwa makosa ya uhalifu dhidi ya dola. Bw Otto Warmbier, mwenye umri wa miaka 21, alikiri kuiba bango la kisiasa katika hoteli alimokuwa akikaa pamoja na kundi jingine la watalii mjini Pyongyang. Marekani imeitaka Korea Kaskazini kumwachilia huru mwanafunzi huyo mara moja.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment