Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, March 19, 2016

Mshukiwa mkuu wa shambulio la Paris akamatwa

Maafisa wa polisi nchini Ubelgiji wakimkamata mshukiwa Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameonya kuwa mitandao ya kigaidi barani Ulaya inaendelea kuimarika licha ya kukamatwa kwa mmoja wa washukiwa wa mashambulizi ya mwezi Novemba mjini Paris. Salah Abdeslam alikamatwa wakati wa uvamizi uliofanywa na kikosi cha kupambana na ugaidi nchini Ubelgiji katika wilaya ya Molenbeek mjini Brussels baada ya kupigwa risasi kwenye mguu. Mtu mwingine ambaye pia anashukiwa kuhusika kwenye mashambulizi hayo ya mwezi Novemba alijeruhiwa na kukamatwa na kwa ujumla watu watano walikamatwa. Bwana Hollande alisema kuwa vita havitakwisha hadi kila mmoja aliyehusika kwenye shambulizi la Paris akamatwe. Watu 130 waliuawa wakati wa shambulizi hilo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment