Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, March 20, 2016

Moja kwa Moja: Uchaguzi wa marudio Zanzibar

14:00 Wawafahamu wagombea wote wa urais walio kwenye karatasi za kura visiwani Zanzibar? Kuna wagombea 14. Majina yao ndiyo haya: 1 Khamis Iddi Lila ACT-W 2 Juma Ali Khatib ADA-TADEA 3 Hamad Rashid Mohamed ADC 4 Said Soud Said AFP 5 Ali Khatib Ali CCK 6 Ali Mohamed Shein CCM 7 Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA 8 Seif Sharif Hamad CUF 9 Taibu Mussa Juma DM 10 Abdalla Kombo Khamis DP 11 Kassim Bakar Aly JAHAZI 12 Seif Ali Iddi NRA 13 Issa Mohammed Zonga SAU 14 Hafidh Hassan Suleiman TLP 13:00 Mji Mkongwe (Stone Town) ambao ni maarufu sana kwa watalii hauna watu wengi. Mwandishi wa BBC Tulanana Bohela amepiga picha hizi zinazoonesha mtaa huo ukiwa kama mahame. 11:15 Mwandishi wa BBC Halima Nyanza aliyeko Zanzibar anasema idadi ya watu waliojitokeza katika baadhi ya vituo ni ndogo, tofauti na uchaguzi wa awali Oktoba 25, mwaka jana. Baadhi ya mitaa imeonekana kutulia huku ulinzi ukiwa umeimarishwa katika baadhi ya maeneo. 10:30 Mgombea urais wa chama cha ADC Hamad Rashid amepiga kura yake kituo cha Tondooni Wawi wilaya ya Chake-Chake, mkoa wa Kusini Pemba. Amesema: "Nina imani ya kuwa Rais, nikikosa nitakuwa Makamu wa Rais". 10:00 Mwanamke akitumbukiza kura kwenye kijisanduku kituo cha Kiembe, Samaki. Upigaji kura unaendelea. 08:50 Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar Dkt Ali Mohammed Shein amezungumza na wanahabari baada ya kupiga kura yake katika kituo cha Bungi, Kibera kisiwani Unguja. Mwanzo amezungumzia hatua ya Chama cha Wananchi (CUF) kususia uchaguzi huo. Kuhusu amani na utulivu, amesema anaamini kutakuwa na utulivu visiwani. Hauhitaji Media PlayerPata usaidizi kuhusu Media PlayerBonyeza 'Enter' kuendelea au kurejea mwanzoni 08:13 Kumbuka, Chama cha Wananchi (CUF) kilitangaza kwamba hakitashiriki uchaguzi wa marudio unaoendelea leo. Chama hicho kinaamini kilishinda uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba mwaka jana na mgombea wake Maalim Seif Hamad anafaa kutangazwa mshindi. Tume ya uchaguzi Zanzibar hata hivyo ilitangazwa kwamba hakuna aliyejiondoa rasmi kutoka kwa uchaguzi wa leo. Lubuva: Magufuli hafai kuingilia kati Zanzibar 08:00 Maafisa wa usalama wakishika doria mjini Chake kisiwani Pemba.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment