Writen by
sadataley
7:40 AM
-
0
Comments
Mahakama moja nchini Brazil imesimamisha uteuzi wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Luiz Inacio Lula da Silva kama mkuu wa utumishi wa uma na mrithi wake Dilam Rousseff.
Agizo hilo la mahakama mjini Brasilia linajiri mda mfupi baada ya Lula kuapishwa katika wadhfa huo.
Mapema ,wafuasi wake na wale wanaompinga walifanya maandamano nje ya jumba la rais.
Wakosoaji wa Lula wanamtuhumu kwa kuchukua wadhfa huo ili kukwepa mashtaka ya ufisadi yanayomkabili.
Kulikuwa na maandamano katika miji kadhaa ya Brazil usiku kucha.Rais Rousseff anakabiliwa na kashfa kubwa ya ufisadi kufuatia madai ya kutoa hongo yanayhusishwa na kampuni kubwa ya mafuta ya Petrobras.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments
Post a Comment