Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, February 26, 2016

Daktari mkeketaji apokonywa leseni Misri

Mahakama nchini Misri hatimaye imempokonya leseni daktari aliyepatikana na hatia ya mauaji ya kutokusudia ya msichana wa miaka 13 ambaye alifariki baada ya kufanyiwa ukeketaji. Raslan Fadl alikuwa daktari wa kwanza nchini Misri kuwahi kushtakiwa na ukeketaji,hata baada ya uovu huo kupigwa marufuku 2008. Hukumu yake ya miaka 2 jela ilipongezwa kuwa ushindi mkubwa na wanaharakati wanaokabiliana na ukeketaji. Lakini ripoti za hivi karibuni zilisema kuwa Fadl hakufungwa na kwamba bado alikuwa anaendelea kuhudumu kama daktari. Licha ya marufuku hiyo ,zaidi ya wasichana asilimia 90 na wanawake walio na umri wa kati ya miaka 15 na 59 nchini humo wamekeketwa katika miaka ya hivi karibuni ,kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment