Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, August 31, 2015

MASPIKA WA MABUNGE DUNIANI WAKUTANA UMOJA WA MATAIFA

Na Mwandishi Maalum, New York Mkutano wa Nne unaowakutanisha Maspika 180 na Manaibu Spika 35 kutoka nchi 140, unaanza leo ( jumatatu) hapa Makao Mkuu ya Umoja wa Mataifa. Mkutano huu wa siku tatu na ambao umeandaliwa na Chama cha Mabunge Duniani ( IPU), utafunguliwa na Rais wa IPU Bw. Chowdhury Saber na Katibu Mkuu wa Umoja wa Matafa, Ban Ki Moon. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Ann Makinda anaongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu. Mkutano ambao Maspika wanatarajiwa kujadiliana kwa kina namna ya kukabiliana na changamoto za Amani, Demokrasia na Maendeleo kwa maono ya Kibunge. Mkutano wa Nne wa Maspika, ulitanguliwa na Mkutano wa Kumi wa Maspika wanawake, mkutano uliofanyika kwa siku mbili ( jumamosi na Jumapili). Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Ann Makinda ameshiriki kikamilifu na kuongoza baadhi ya mikutano. Mkutano wa Nne wa Maspika ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya Maspika hao na ambayo imekuwa ikifanyika kuelekea Mkutano wa Kilele wa Viongozi wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika wiki chache zijazo ambapo watapokea na kupitisha Ajenda Mpya za Maendeleo Endelevu baada ya 2015. Chanzo: CCM Blog
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment