Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 31, 2015

Nigeria yateua General mpya

Rais wa Nigeria Mhamadu Buhari Nigeria imemteua Generali mpya kuongoza kikosi cha kimataifa kilichoundwa kwa ajili ya kupamba na kundi la wanamgambo wa Boko Haram. Meja General Iliyasu Isah Abbah ataongoza kikosi hicho kitakachokuwa na askari takriban 9000 kutoka nchi tano. Nigeria imemchagua General huyo mpya kwa lengo la kupambana na wanamgambo hao wa kundi la kigaidi la Boko Haram. Kikosi hicho kinatarajiwa kuwa na ofisi zake katika mji mkuu wa Chad N'Djamena na wanatarajiwa kuendesha operesheni zake kikamilifu kuanzia mwezi ujao. Nigeria na majirani zake wamekuwa wanajitahidi kupambana na wapiganaji wa Boko Haram ambao wameua watu wapatao elfu ishirini. Chanzo:BBC Swahili
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment