Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 31, 2015

Burundi:Agathon Rwasa ni naibu wa spika

Agathon Rwasa achaguliwa naibu spika wa bunge la Burundi Hii leo bunge lipya lililochaguliwa nchini Burundi limewateua viongozi wake. Licha ya kupinga uchaguzi mkuu wa hivi majuzi kiongozi wa upinzani Agathon Rwasa amekubali kuwa naibu wa spika. Wadhifa wa spika umekabidhiwa mwenyekiti wa chama kinachotawala CNDD FDD Pascal Nyabenda. Rwasa alijipatia kura 108 kati ya 112 baada ya kupata uungwaji mkono na chama cha CNDD-FDD. Baada ya uteuzi wa leo, imebainika wazi kuwa uongozi wa bunge hilo utatawaliwa na wanaume kutokana na kuondolewa sheria ya ndani walioweka kuwa lazima kuwe na uakilishi wa wanawake japo mmoja, katika uongozi wa bunge hilo. Rwasa alijipatia kura 108 kati ya 112 baada ya kupata uungwaji mkono na chama cha CNDD-FDD. Zaidi ya watu 70 walipoteza maisha yao baada ya makabiliano kati ya wafuasi wa rais Pierre Nkurunziza na wapinzani waliomtaka asigombee kiti muhula wa tatu wa urais. Rais Nkurunziza alishinda kwa asilimia 70 ya kura Wapinzani walidai kuwa muhula huo unakiuka sheria za nchini. Naye rais Nkurunziza alishikilia kuwa muhula wa kwanza hakuchaguliwa na watu ,kwa hivyo haikuwa kinyume na sheria kwake kuwania muhula mwengine wa urais. Chanzo:BBC Swahili
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment